Saturday, January 11, 2014

WATU watatu wanaosadikiwa kuwa majambazi wameuawa kwa kuchomwa moto usiku wa kuamkia leo baada ya kuvamia dukal a mama mmoja wa kijiji cha Kisiwa, kata ya Kiloka, wilaya ya Morogoro Vijijini.


MAJAMBAZI WATATU WAUAWA MORO VIJIJINI

WATU watatu wanaosadikiwa kuwa majambazi wameuawa kwa kuchomwa moto usiku wa kuamkia leo baada ya kuvamia dukal a mama mmoja wa kijiji cha Kisiwa, kata ya Kiloka, wilaya ya Morogoro Vijijini.
Jumla ya majambazi hao walikuwa 10 ambapo saba walifanikiwa kutokomea na watatu kutiwa nguvuni na wananchi wenye hasira kali walioamua kuwatia moto!

LULU AMSHANGAZA MAMA KANUMBA

Stori: Hamida Hassan na Imelda Mtema

MSANII wa filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’, mwanzoni mwa wiki hii alimshangaza (surprise) mama wa mpenzi wake wa zamani, marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa wakati alipokuwa akisherehekea miaka 58 tokea alipozaliwa.
Keki aliyoleta Lulu kwa ajili ya mama Kanumba.
Kumshangaza huko kumekuja baada ya Lulu kufika nyumbani kwa mama Kanumba, Kimara Temboni jijini Dar akiwa na bonge la keki, jambo ambalo mama huyo hakulitarajia.…
Stori: Hamida Hassan na Imelda Mtema
MSANII wa filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’, mwanzoni mwa wiki hii alimshangaza (surprise) mama wa mpenzi wake wa zamani, marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa wakati alipokuwa akisherehekea miaka 58 tokea alipozaliwa.
Keki aliyoleta Lulu kwa ajili ya mama Kanumba.
Kumshangaza huko kumekuja baada ya Lulu kufika nyumbani kwa mama Kanumba, Kimara Temboni jijini Dar akiwa na bonge la keki, jambo ambalo mama huyo hakulitarajia.
Lulu akimpatia keki mama Kanumba.
“Yaani mama Kanumba alikuwa hajui kuwa Lulu anajua siku yake ya kuzaliwa, Lulu akatumia nafasi hiyo kumfanyia ‘sapraizi’,” alisema rafiki wa karibu wa Lulu aliyeomba hifadhi ya jina lake.
...Lulu akimlisha keki mama Kanumba.
Waandishi wetu waliokuwa eneo la tukio walimshuhudia mama Kanumba akiwa amepigwa na butwaa huku akilengwalengwa na machozi ya furaha. Mahojiano yalifanyika kama ifuatavyo;
Ijumaa: Hongera mama, sasa unatimiza miaka mingapi?
Mama Kanumba: Nimetimiza miaka 58.
Mama Kanumba akimlisha keki mama mzazi wa Lulu, Lucresia Karugila.
Ijumaa: Umejisikiaje kwa zawadi ya keki uliyoletewa na Lulu?
Mama Kanumba: Nimejisikia furaha sana kwa kweli, Lulu ni mwanangu, nimefarijika, kwa sababu watoto wangu hawapo, leo ningekuwa peke yangu lakini kama unavyoona, mama na mwanaye wamekuja toka asubuhi tunasherehekea nao kwa kula na kunywa na Lulu amegharamia kila kitu.
Baada ya swali hilo Ijumaa lilihamia kwa Lulu.
Kutoka kushoto: Flora Mtegoa, Lulu na Lucresia Karugila katika pozi.
Ijumaa: Ulijuaje leo ni siku ya kuzaliwa ya mama Kanumba?
Lulu: Nilijua katika maongezi siku sita zilizopita, kwani ilikuwa ni tarehe moja ya mwezi huu ambapo amezaliwa mama yangu mzazi na dada yangu.
Ijumaa: Kwa nini uliamua kumfanyia Sapraizi ya keki mama Kanumba?
Mama Kanumba akikata keki.
Lulu: Niliamua kumfurahisha kwa sababu ni siku yake ya kuzaliwa na sikufanya kwa sababu mwanaye hayupo, hata angekuwepo ningemfanyia tu.
Ijumaa: Asanteni, mama na Lulu tunawatakia maisha mema.
Flora Mtegoa akipozi na Lulu.

MASOGANGE ANASWA NA BWANA WA JACK

Na Mwandishi Wetu

VIDEO Queen, Agnes Jerald ‘Masogange’ hivi karibuni alibambwa maeneo ya Sinza Kamanyola jijini Dar akijiachia na anayetajwa kuwa ni mpenzi wa Jack Patrick, Juma Khalid ‘Jux’.
Masogange akipozi na Jux.
Wawili hao walibambwa kwenye duka moja lililopo maeneo hayo baada ya Jux kutua kutoka China huku Agnes akionekana kama anayemfariji kwa tukio la Jack kunaswa na madawa ya kulevya.
http://api.ning.com/files/Iht4Psekqy0wttdXe*EsPRkqo*eRW*Qp69gUzbFS7smv8PTpbqof801LuB2JiAsnEHN0DmKCmtkMNQ9uNA-PB4Cq4PCBRIbh/jacknajux.jpg%3Fwidth%3D650 Jux akiwa na mpenzi wake…
Na Mwandishi Wetu
VIDEO Queen, Agnes Jerald ‘Masogange’ hivi karibuni alibambwa maeneo ya Sinza Kamanyola jijini Dar akijiachia na anayetajwa kuwa ni mpenzi wa Jack Patrick, Juma Khalid ‘Jux’.
Masogange akipozi na Jux.
Wawili hao walibambwa kwenye duka moja lililopo maeneo hayo baada ya Jux kutua kutoka China huku Agnes akionekana kama anayemfariji kwa tukio la Jack kunaswa na madawa ya kulevya.
http://api.ning.com/files/Iht4Psekqy0wttdXe*EsPRkqo*eRW*Qp69gUzbFS7smv8PTpbqof801LuB2JiAsnEHN0DmKCmtkMNQ9uNA-PB4Cq4PCBRIbh/jacknajux.jpg%3Fwidth%3D650Jux akiwa na mpenzi wake Jack Patrick.
Akiuzungumzia ukaribu wake na Jux, Masogange alisema: “Wala hakuna lolote kati yangu na yeye. Mimi na wale akina Jux pamoja na dada yake ni watu wangu wa karibu sana tunaojuana muda mrefu hivyo tulikuwa  tunabadilishana mawazo tu.”
Masogange akiwa na Jack.
Jux na Jack wamekuwa wakionekana katika mitaa ya China wakila bata huku kukiwa na madai kuwa ni wapenzi na kuonekana kwa Jux na Masogange wakijiachia kumeibua maswali mengi.


MREMBO AZUA KASHESHE, KISA WIVU WA MAPENZI!


Mrembo akizua kasheshe baada ya kutolewa nje ya Ukumbi wa Mango Garden, Mwananyamala, Dar.
Stori: Issa Mnally

AMA kweli pombe siyo chai. Timbwili la aina yake liliibuka ndani ya Ukumbi wa Mango Garden, Mwananyamala jijini Dar hivi karibuni baada ya dada mmoja kuanzisha kasheshe alipomkuta mpenzi wake akiwa amekaa kimahaba na demu mwingine.…

Mrembo akizua kasheshe baada ya kutolewa nje ya Ukumbi wa Mango Garden, Mwananyamala, Dar.
Stori: Issa Mnally
AMA kweli pombe siyo chai. Timbwili la aina yake liliibuka ndani ya Ukumbi wa Mango Garden, Mwananyamala jijini Dar hivi karibuni baada ya dada mmoja kuanzisha kasheshe alipomkuta mpenzi wake akiwa amekaa kimahaba na demu mwingine.
Mrembo akiwa mikononi mwa baunsa.
Kisa kizima kilichoshuhudiwa na paparazi wetu kilitokea majira ya saa 8:00 usiku baada ya dada huyo kwenda kujisaidia msalani na aliporudi akamkuta mpenzi wake akiwa ameinamiwa na demu mwingine kimahaba.
...Akitolewa nje ya ukumbi na baunsa.
Dada huyo alipomuona mpenzi wake anamsomesha demu mwingine, hakukubali akamrukia yule demu aliyekuwa akizungumza na mpenzi wake na kuwafanya wote kuanguka chini ndipo timbwili lilipoanza.
...Twende nje.
Hata hivyo, timbwili hilo halikudumu kwa muda mrefu kwani walinzi wakiwemo mabaunsa walifanya kazi ya ziada kumtoa dada huyo ukumbini hapo huku akiwa hana viatu.
...Mrembo akitaka kurudi tena.
Hata hivyo, katika kuepusha vurugu zaidi, walinzi wa eneo hilo walimuomba mpenzi wa sistaduu huyo naye atoke nje ili wakamalize ugomvi wao kisha waende wakalale.
...Akizidi kukinukisha.

JOHARI AWARUSHA ROHO RAY, CHUCHU HANS

Stori: SHAKOOR JONGO

HUKU Ray na Chuchu Hans wakionekana penzi lao limepamba moto, mpenzi wa zamani wa  Ray, Blandina Chagula ‘Johari’ ameonekana kuwarusha roho wawili hao baada ya kutupia mtandaoni picha inayomuonesha kidoleni amevaa pete ya ndoa.
Johari.
Wakizungumza na Ijumaa baadhi ya watu waliobahatika kuiona picha hiyo wamesema kuwa kitendo cha Johari kuweka picha hiyo ni sawa na kuwarusha roho wawili hao kwamba yeye atakuwa wa kwanza kuolewa kabla ya Chuchu na Ray kufunga ndoa.…
Stori: SHAKOOR JONGO
HUKU Ray na Chuchu Hans wakionekana penzi lao limepamba moto, mpenzi wa zamani wa  Ray, Blandina Chagula ‘Johari’ ameonekana kuwarusha roho wawili hao baada ya kutupia mtandaoni picha inayomuonesha kidoleni amevaa pete ya ndoa.
Johari.
Wakizungumza na Ijumaa baadhi ya watu waliobahatika kuiona picha hiyo wamesema kuwa kitendo cha Johari kuweka picha hiyo ni sawa na kuwarusha roho wawili hao kwamba yeye atakuwa wa kwanza kuolewa kabla ya Chuchu na Ray kufunga ndoa.
Ray na Chuchu.
“Unajua kila mtu ana njia yake ya kufikisha ujumbe, kitendo cha hivi juzi Ray na Chuchu kujiachia bila ya kificho katika Viwanja vya Leaders Club, ambapo kulikuwa na uchaguzi wa viongozi wa Bongo Movie ni sawa na kumwambia Johari hana chake ndiyo maana na yeye ameamua kurudisha kijembe kwa staili ya kuweka picha aliyovaa pete ya ndoa ili kuonyesha kuwa yeye ataolewa ila Chuchu atachezewa tu na kutupwa,” alidai mmoja wao.
Baada ya kusikia taarifa hizo kutoka kwa wadaku hao Ijumaa lilimuendea hewani Johari ambapo alipokea simu na kusema atafutwe muda mwingine kwani  alikuwa yupo bize.

SANDRA NA RUSHWA YA NGONO BONGO MOVIE

Stori: Mayasa Mariwata

STAA wa filamu Bongo, Salma Salmini ‘Sandra’ amesema kuwa tangu ajiunge Bongo Movie hakuna manufaa aliyoyapata kwa kuwa chama hicho kinaendekeza ubaguzi kwa kuthamini rushwa ya ngono.
Salma Salmini ‘Sandra’.
Akipiga stori na paparazi wetu alisema, kikubwa kinachoikwamisha tasnia hiyo ambayo kwa sasa inaongozwa na Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ ni watu kusaidiana wenyewe kwa wenyewe kwa kuwa labda wanatoka kimapenzi au kutegemea kupewa rushwa ya ngono ili impe shavu mtu.
“Namsihi…
Stori: Mayasa Mariwata
STAA wa filamu Bongo, Salma Salmini ‘Sandra’ amesema kuwa tangu ajiunge Bongo Movie hakuna manufaa aliyoyapata kwa kuwa chama hicho kinaendekeza ubaguzi kwa kuthamini rushwa ya ngono.
Salma Salmini ‘Sandra’.
Akipiga stori na paparazi wetu alisema, kikubwa kinachoikwamisha tasnia hiyo ambayo kwa sasa inaongozwa na Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ ni watu kusaidiana wenyewe kwa wenyewe kwa kuwa labda wanatoka kimapenzi au kutegemea kupewa rushwa ya ngono ili impe shavu mtu.
“Namsihi sana huyu kiongozi wetu wa sasa awe makini na hili suala, yeye pamoja na utawala wake wote wapinge haya mambo na tushikamane ile kuleta maendeleo, maana kila siku wanaopewa madili ya maana ni walewale lakini wengine tunaheshimika kwa majina tu huku dhiki zikitutawala,” alisema Sandra.


BASI LA MTEI LATEKETEZWA KWA MOTO BAADA YA KUGONGA NA KUUA SINGIDA

Basi la mtei likiteketea kwa moto baada ya kuchomwa na watu wenye hasira kali.…
Basi la mtei likiteketea kwa moto baada ya kuchomwa na watu wenye hasira kali.
Muonekano wa basi la Mtei baada ya kuzimwa moto huo.
Habari ambazo mtandao huu umezipata kutoka Singida zinasema Basi la abiria la Matei linalofanya safari zake kutoka Mwanza kwenda Dar  limechomwa moto na kuteketea kabisa na watu wenye hasira kali baada ya kugonda bodaboda ambayo ilikuwa imepakia ‘mshikaki’ wa watu watatu ambao walikufa papohapo eneo la tukio.
Hakuna abiria wa basi aliyeumia.  Mwandishi wetu aliye kwenye tukio amesema Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Singida, Geofrey Kamwela yupo eneo ya tukio akishughulikia sakata hilo.

SOMA HAPA MAGAZETI YA LEO TAREHE 10 JANUARY 2014: FUMANIZI SALOON




Stori: WAANDISHI WETU

AMA kweli shetani anafanya hesabu zake za mwisho! Tangu mwaka 2014 uanze yapo yaliyotokea na kusisimua likiwemo la kunaswa kwa kinara wa utoaji mimba, Dk. Mambo, maeneo ya Kawe, Dar lakini hili la warembo kufumwa wakitoa dozi ya ngono linaweka historia nyingine, Ijumaa linaibumburua.
Warembo wanaotoa huduma wakiwa wameficha sura zao baada ya kunaswa na OFM.
Hebu sikia, saluni inayojihusisha na vitendo vya ’masaji’ lakini kumbe ngono imo ndani yake imenaswa na kufumuliwa baada ya kukutwa uchafu…
Stori: WAANDISHI WETU
AMA kweli shetani anafanya hesabu zake za mwisho! Tangu mwaka 2014 uanze yapo yaliyotokea na kusisimua likiwemo la kunaswa kwa kinara wa utoaji mimba, Dk. Mambo, maeneo ya Kawe, Dar lakini hili la warembo kufumwa wakitoa dozi ya ngono linaweka historia nyingine, Ijumaa linaibumburua.
Warembo wanaotoa huduma wakiwa wameficha sura zao baada ya kunaswa na OFM.
Hebu sikia, saluni inayojihusisha na vitendo vya ’masaji’ lakini kumbe ngono imo ndani yake imenaswa na kufumuliwa baada ya kukutwa uchafu wa aina yake nyuma ya pazia.
Saluni hiyo maarufu kuliko Miji ya Sodoma na Gomora, ipo maeneo ya Sinza ambapo kwa muda mrefu sasa imekuwa ikijihusisha na uchafu huo na kusababisha kero kwa wananchi wenye maadili yaliyotukuka.
TAARIFA MEZANI
Oparesheni Fichua Maovu (OFM) chini ya Global Publishers, ikiwa imetulia ndani ya mjengo wa makao yake makuu, Bamaga-Mwenge jijini Dar, Mkuu wa kikosi maalumu cha Mtambo wa Kurekebisha Tabia (MKT) ambacho ni kitengo ndani ya OFM, alipokea simu kutoka kwa msamaria mwema akitoa ‘tipu’ juu ya ishu hiyo.
Mhudumu baada ya kumpatia dozi mteja.
Mtoa taarifa huyo alieleza malalamiko yake juu ya kero wanayoipata raia waishio jirani na saluni hiyo kufuatia huduma chafu za kuchukiza ambazo hufurahiwa na shetani na malaika wake tu.
Msamaria Mwema: Halooo.... halooo... jamani halooooo, hapo ni Makao Makuu ya OFM?
OFM: Ndiyo mama, tukusaidie nini?
Msamaria Mwema: Mna habari jamani?
OFM: Zimejaa tele, ila hata ya kwako inaweza kuwa bora kuliko tulizonazo.
Msamaria Mwema: Hapa Sinza Kwaremi (Dar) kuna saluni moja inaendesha vitendo vichafu vya ngono na hakuna sheria yoyote inayochukuliwa dhidi ya wahusika.
...Huyu alinaswa akikimbia baada ya OFM kutia maguu eneo la tukio.
OFM: Saluni ya ngono? Kivipi mama? Hebu fafanua tafadhali!
Msamaria Mwema: (kwa sauti ya juu mno) ninyi njooni mtajua kila kitu hukuhuku lakini inaendesha mambo ya ajabu (simu ikakatika).
OFM MZIGONI
Bila kupoteza sekunde, mkuu huyo wa MKT, aliwapanga ‘makamanda’ maalumu na kuwapa maelekezo muhimu ya jinsi ya kujua ukweli juu ya uovu uliodaiwa kutendwa kwenye saluni hiyo.
UCHUNGUZI
OFM iliwatuma vijana wake ‘watanashati’ hadi eneo lililotajwa ili wachunguze kama kweli kuna saluni yenye jina lililotajwa na mtoa habari wetu.
Baada ya maelekezo hayo, vijana hao wakiongozwa na roho safi ya kunyoosha maadili katika jamii, walifika hadi Sinza na kukuta saluni yenye jina hilo ambapo walianza kufanya upelelezi wa hali ya juu mno huku wakiwa makini kuliko hata neno lenyewe.
UTHIBITISHO
Baada ya kutinga eneo hilo, OFM iliendesha upelelezi maalumu kwa kuwauliza baadhi ya wakazi na watu wanaofanyia shughuli zao za kujiingizia riziki na kupata ukweli halisi juu ya ufuska ufanywao ndani ya saluni hiyo.
Katika uchunguzi huo, OFM ilipata uthibitisho kuwa kweli ibilisi yuko katika hesabu zake za mwaka kwa kufanya uchafu wa kufuru.
Ilielezwa kwamba, watumishi wa saluni hiyo ambao ni warembo, hujifanya wanatoa huduma ya kuchua mwili (body massage) kwa Sh. 25,000/= kwa vyumba na huduma za kawaida, lakini kwa vyumba vyenye choo na bafu kwa ndani (self contained) ni Sh. 35,000/=.
HUDUMA
Katika upelelezi huo, ilibainika kuwa mteja akilipia gharama ya vyumba vya self contained, ana uhuru wa kuchagua kama atapenda kufanyiwa huduma ya uchuaji kwa mikono tu au kwa matiti na wakati mwingine mwili mzima huku mtoa huduma hiyo akiwa amevua nguo zote!
Ikazidi kuelezwa kuwa, endapo mhudumiwaji atataka huduma hiyo ya mchuaji kuvua nguo zote, atafanyiwa hivyo lakini kama atazidiwa na kuhitaji huduma ya ngono, atatakiwa kuongeza Sh. 50,000/= kwa msichana huyo wa huduma na kufanya gharama kuwa zaidi ya Sh. 80,000/=.
“Wamekuwa wakifanya vitendo viovu sana, yaani ngono njenje, jamani hii siyo saluni, bali ni danguro la ngono fuatilieni mtangundua juu ya ukweli huu,” alisema mmoja wa raia katika upelelezi wa OFM.
OFM NDANI YA NYUMBA
Ili kujiridhisha na maelezo hayo, timu ya OFM ilituma vijana wake tofauti kwa muda wa siku tatu mfululizo na kubaini kuwa yote yaliyosemwa na kutajwa kwa kirefu yanatendeka ndani ya saluni hiyo!
‘Askari’ wa kwanza wa OFM aliingia ndani ya saluni hiyo (jina linavunda kwenye droo za meza yetu) na kuwakuta wahudumu wamejaa tele na alipowauliza juu ya huduma ya masaji na ngono, walijibu kwa sauti ya furaha na bashasha kubwa bila kujua kuwa kijana wetu alikuwa na vifaa maalumu vya kunasia sauti.
“Ni wewe tu jamani, kwani wewe ni mgeni maeneo haya? Mbona utaratibu unaeleweka, lakini maelezo ni hayo kwa hiyo karibu sana,” alisema mmoja wa warembo hao huku akilegeza macho mithili ya mgonjwa wa degedege.
Siku mbili zilizofuata, askari wa OFM waliendelea kupata stori na maelezo ya aina hiyohiyo.
MTEGO!
Siku ya tukio, (mwanzoni mwa wiki hii) OFM iliweka mtego kwa kumpeleka kijana wake ili ajifanye anahitaji huduma hiyo ya kufanyiwa masaji mwili mzima na baadaye ajifanye amezidiwa na kuhitaji huduma ya ngono.
Katika mtego huo, OFM ilitoa taarifa polisi ambapo ‘vijana wa IGP Ernest Mangu’ hawakulaza damu, wakatoa ushirikino wa kutosha kwa OFM.
MTEGO WAFYATUKA
Kama kawaida, OFM huwa haishindwi linapokuja suala la oparesheni maalumu kama hiyo, fuatilia sana. Mtego wake ulifyatuka ambapo mmoja wa vijana wake alijifanya kuhudumiwa (angalia picha ukurasa wa mbele).
Baada ya kuweka mazingira sawa, OFM na polisi wa kike na kiume walivamia na kufanikiwa kufuma laivu matukio mengi ya ufuska mkubwa (ukitaka kuona zaidi, unakaribishwa Bamaga ofisini kwetu).
WAUME ZA WATU!
Baada ya zoezi hilo kukamilika, baadhi ya mashuhuda (hasa akina mama) walisikika wakishukuru kufumuliwa kwa saluni hiyo kwa kuwa ndoa zao zilikuwa zimeanza kuota magugu kwani wateja wengi wa saluni hiyo ni waume za watu na vigogo serikalini!
“Jamani tunashukuru sana, waume zetu walikuwa wanakimbilia hapo, ugomvi kidogo tu, mwanaume anakwenda hapo na akirudi nyumbani hana habari kabisa na mkewe, safi sana OFM na polisi kwa jumla,” alisikika mama Joyce akishangilia kufumuliwa kwa saluni hiyo.
SOO POLISI
Baada ya ‘sheshe’ hilo, warembo sita walikamatwa na kupelekwa kituo cha polisi kwa upelelezi maalumu.
MMILIKI
Katika upelezi wa awali, watumishi hao walimtaja mmiliki wa saluni hiyo kwa jina moja la Chifu huku wakishindwa kuweka wazi na kufafanua kwa undani zaidi.
KAMANDA WAMBURA UPO?
Gazeti hili lilifanya jitihada za hali ya juu kumpata Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, ACP Camilius Wambura ili azungumzie juu ya sakata hilo, lakini hadi gazeti hili linakwenda mitamboni, simu yake ya kiganjani ilikuwa ikiita bila kupokelewa.
KUTOKA IJUMAA:
Timu nzima ya OFM na dawati la Ijumaa kwa jumla, tunalaani vikali kuwepo kwa vitendo viovu kama hivi vinavyokwenda kinyume na maadili na utamaduni wetu kwa sababu vinachochea mmomonyoko wa maadili na ongezeko la maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi.

HATA KAMA YUKO MBALI, UNAWEZA KUWA KARIBU NAYE! - 2


UMBALI katika uhusiano, mara nyingi husababisha hofu. Fikra za usaliti hutawala sana kwa wenzi wanaoishi mbali. Lakini vipi, mwenzako asisafiri au asiishi mbali kwa kuhofia hayo wakati kitendo hicho kinasababishwa na jukumu la kikazi?
Ndugu zangu, baadhi yetu, kama hatutakuwa makini, umbali huweza kuchochea usaliti. Lakini kuna njia ambazo zikitumika kwa usahihi, husaidia kuliweka penzi hai na kuzidi kuwa na mshawasha mkubwa.
Wiki iliyopita nilianza kwa kueleza umuhimu wa mawasiliano, hasa simu, waraka pepe na mitandao ya kijamii. Kuweka utani kwa mwenzako, kusoma ratiba yake na kuishika siku yake sawasawa kunamfanya mwezako…
UMBALI katika uhusiano, mara nyingi husababisha hofu. Fikra za usaliti hutawala sana kwa wenzi wanaoishi mbali. Lakini vipi, mwenzako asisafiri au asiishi mbali kwa kuhofia hayo wakati kitendo hicho kinasababishwa na jukumu la kikazi?
Ndugu zangu, baadhi yetu, kama hatutakuwa makini, umbali huweza kuchochea usaliti. Lakini kuna njia ambazo zikitumika kwa usahihi, husaidia kuliweka penzi hai na kuzidi kuwa na mshawasha mkubwa.
Wiki iliyopita nilianza kwa kueleza umuhimu wa mawasiliano, hasa simu, waraka pepe na mitandao ya kijamii. Kuweka utani kwa mwenzako, kusoma ratiba yake na kuishika siku yake sawasawa kunamfanya mwezako asikusahau na wakati fulani ahisi kukukosa.
Hebu sasa tuendelee...
ZAWADI
Zawadi ni kati ya mambo ambayo humfanya mpenzi wako afurahie uhusiano wake na wewe. Hakuna zawadi za moja kwa moja ambazo ni rasmi kwa ajili ya mwenzi wako, lakini ni vyema ukamtumia zawadi kulingana na mapenzi yake zaidi.
Kwakuwa wewe unamfahamu zaidi mwenzi wako, unaweza kujua zawadi gani ni nzuri zaidi kwake au anayopendelea kuliko aina nyingine. Katika vijipengele vifuatavyo, nimechambua aina kuu za zawadi ambazo ukimtumia mpenzi wako unamteka hisia zake na kuona kama yupo karibu na wewe hata kama yupo mbali.
(i) Mavazi
Mavazi ni kati ya zawadi ambazo zitamfanya mpenzi wako azidi kukupenda na kuwa karibu zaidi na wewe. Kama nilivyotangulia kusema awali, aina ya nguo ambazo unaweza kumtumia mpenzi wako ni zile ambazo unadhani atavutiwa nazo zaidi au zile ambazo zitampendeza na kumfanya aonekane nadhifu.
Hata hivyo, zipo aina za mavazi ambazo zimependekezwa zaidi kwa ajili ya wenzi kutumiana wanapokuwa mbali.
KWA WANAUME: Kama wewe ni mwanamke unataka kumtumia mwenzi wako wa kiume, mavazi haya yanafaa zaidi. Saa nzuri ya mkononi, nguo za ndani, lakini lazima uzingatie rangi ya bluu, bluu bahari au nyeupe kimsingi zisiwe za rangi inayoficha uchafu.
Zingine ni fulana za ndani, tisheti, mkanda wa kiunoni, simu ya mkononi, vitambaa vya jasho n.k. hakikisha katika zawadi zako hizo, unaambatanisha na manukato mazuri (hasa unayotumia wewe).
Haishauriwi kumtumia suruali au shati kwa sababu inaweza kuwa kubwa au ndogo, hivyo kupunguza ladha ya zawadi hasa kama atakuwa ameipenda. Zawadi za aina hiyo, unaweza kumpa mwenzi wako ofa ya kwenda kuchagua moja kwa moja dukani.
KWA WANAWAKE: Kama wewe ni mwanaume na unataka kumtumia mpenzi wako wa kike zawadi, lazima uwe makini sana! Mavazi yaliyopendekezwa hapa ni pamoja na batiki (gauni, blauzi na sketi, blauzi yenyewe n.k), hereni, bangili, mkufu wa vito, simu, saa, nguo za ndani, viatu n.k.
Kama umesoma vizuri utaona mwanamke anaweza kununuliwa vitu vingi zaidi, tofauti na mwanaume. Hii inatokana na aina za mavazi na saizi zao kukaririka kirahisi zaidi au kutokuwa na saizi ya moja kwa moja.
Kama kawaida, mavazi haya ambatanisha na manukato mazuri sana, hasa yale ambayo unapenda kutumia wewe. Ninaposema uweke manukato unayotumia, maana yake itamsaidia kumsogeza karibu zaidi kihisia kwa kuhisi harufu yako.
Wiki ijayo tutaendelea na mada yetu, USIKOSE!
Joseph Shaluwa ni Mshauri wa Mambo ya Mapenzi anayeandikia magazeti ya Global Publishers. Ameandika vitabu vitatu; True Love, Let’s Talk About Love na All About Love vilivyopo mitaani.