Friday, June 6, 2014

Boko Haram wafanya mauaji: zaidi ya watu 20 wameuawa katika mashambulio katika vijiji vya jimbo la Borno.

Hii inatokea wakati bado kuna wasiwasi mkubwa juu ya hatma ya wasichana zaidi ya 200 waliotekwa nyara na kundi hilo yapata siku 50 zilizopita.

Wakaazi wa kijiji cha Attagara karibu zaidi na mpaka wa Cameroon na Nigeria wamesema kuwa watu waliovalia sare za kijeshi walikuja katika kijiji chao na kuwaagiza watu waje katika uwanja wa kanisa.
Wanadai kuwa walidhania watu hao walikuwa wnajeshi wa serikali waliokuja kuwapa ulinzi. Na baada ya wanajeshi hao kuwafyatulia risasai ndipo waligundua kuwa walikuwa wapiganaji wa Boko Haram.
Mbunge wa eneo hilo Peter Biye amethibitishia BBC tukio hilo na kusema kuwa watu wengi wameuawa na nyumba kuchomwa katika vijiji vingine 5 mbali na hicho.

'Jeshi lakanusha madai'
Wakati huo huo jeshi la Nigeria limekanusha madai katika vyombo vya habari kuwa mahakama ya kijeshi nchini humo imewapata na hatia baadhi ya maafisa wakuu wa jeshi kwa kuwasaidia wapiganaji wa Boko Haram.
Msemaji kutoka jeshi hilo amekanusha madai kuwa kuna majenerali 15 wa wa jeshi waliofunguliwa mashtaka ya kuwasaidia magaidi.
Jeshi limesema kuwa taarifa hizo ni batili zilizolenga kulidhalilisha jeshi la nchi hiyo wakati mambo yako tete.
nyumba zimechomwa Borno 

Hali imeendelea kuwa ya wasiwasi miongoni mwa wakaazi wa maeneo mengi kaskazini mashariki mwa Nigeria kutokana na mashambulio yaliyochacha.
Wapiganaji wamekuwa wakishambulia kwa bomu maeneo ya umma na kuwaua watu zaidi ya 200 katika chini ya miezi miwili tu.
Suala la wasichana waliotekwa pia bado limekaa kama mwiba wa samaki kooni mwa serikali ya Nigeria ambapo shinikizo kutoka jamii ya kimataifa zinaendelea kutaka wakombolewe kwa haraka.
Awali serikali ilikuwa imepiga marufuku maandamano yoyote kutokana na tisho la usalama lakini ssa polisi wametangaza kuwa maandamano ya amani yanaweza kufanywa.

Chanzo BBC Swahili

Morogoro: Gari aina ya Prado laacha njia na kuvamia bank ya CRDB jana mapema

Gari aina ya Prado limeacha njia na kupamia bank ya CRDB Mkoani Morogoro. tukio hilo lilitokea mapema sana jana. Ajali hiyo imetokea wakati mmoja wa wafanyakazi wa hapo (Jane Maganga) akipaki gari yake, gari ilipitiliza na kuingia ndani. Hakuna mtu aliye umia katika ajali hiyo.

 Picha ya gari lililo pamia bank


Sehemu iliyogongwa

Wednesday, June 4, 2014

Ukatili unazidi kuendelea: Mwanamke mmoja jina lake halijaweza kufahamika. Amediliki kumuua mtoto na kumtupa barabarani...

Mwanamke mmoja asiyefahamika jina wala sehemu anayoishi amefanya tendo la kinyama kwa kumuua mtoto mchanga mwenye jinsia ya kike kwa kumfunga plasta puani na mdomoni hali iliyompelekea mtoto huyo kushindwa kupumua na kupoteza maisha. Tukio hilo la kikatili limekutwa pembezoni mwa barabara ya Kawe Beach Jiji Dar es salaam


Wavuvi wa eneo hilo waliona mfuko pembeni ukiwa na damu hali iliyowashangaza wakaamua kuusogelea na kukuta kichanga hicho kimefungwa na plasta mdomoni na puani kikiwa kimeshafariki.