Thursday, November 27, 2014

KUTOKA BUNGENI DODOMA LEO: MASWALI KWA WAZIRI MKUU


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
KIKAO cha Bunge leo kimeanza kwa maswali kwa Waziri Mkuu ambapo aliyekuwa wa kwanza kuuliza alikuwa ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Mhe. Freeman Mbowe.


Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Mhe. Freeman Mbowe.
Alianza Mbowe: 
“…Chini ya uongozi wako kama Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ukiwa kiongozi wa…

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

KIKAO cha Bunge leo kimeanza kwa maswali kwa Waziri Mkuu ambapo aliyekuwa wa kwanza kuuliza alikuwa ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Mhe. Freeman Mbowe.

Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Mhe. Freeman Mbowe.
Alianza Mbowe: 
“…Chini ya uongozi wako kama Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ukiwa kiongozi wa shughuli za Kiserikali Bungeni, tumeiona Serikali ikikumbana na matatizo na vikwazo vingi ikiwemo ‘Operesheni Tokomeza’ ambayo ilipelekea wananchi wengi kupoteza maisha na wengine kupata vilema…“
Tumeona mauaji ya raia yakiendelea Kiteto, kashfa kubwa ambayo iko current sasa hivi ikiwa ni pamoja na kauli zako ulizowahi kuzisema kwamba fedha zilizopotea za akaunti ya Escrow hazikuwa fedha za umma bali zilikuwa fedha za watu binafsi…“– Mbowe.
Baada ya Ripoti ya CAG kutolewa hadharani kuhusiana na fedha za Akaunti ya Escrow na baada ya Ripoti ya PCCB kutolewa na hatimaye jana hapa Bungeni kusomwa taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), nini msimamo wako kuhusu kauli yako ya awali kwamba fedha zile zilikuwa ni za watu binafsi na sio fedha za umma?“– Mbowe.
Kwa uzito huo ukichanganya na matukio mengine mbalimbali ambayo yamepelekea fedheha kubwa kwa taifa letu, huoni kama ingekuwa muafaka kwako binafsi na taifa kupumzika kidogo ili kupisha nafasi kwa watu wengine kuweza kumalizia ngwe hii ya utawala wenu?”– Mbowe.
Akijibu maswali hayo, Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema; “…Inawezekana Mheshimiwa Mbowe una shauku ya kutaka litokee hilo lakini mambo haya yanategemea kama ndivyo Mungu kapanga au hapana…“
Ningeweza nikajaribu kukujibu lakini sina sababu ya kufanya hivyo, sina sababu ya kufanya hivyo kwa sababu suala lenyewe ndiyo subject ya mjadala hapa Bungeni ambao unaanza leo.. Tusubiri mjadala utakavyokwenda naamini na mimi nitapata nafasi ya kusema mawili matatu, kwa hiyo nadhani mwisho wa yote Bunge litakuwa limefikia mahali ambapo tunaweza tukasema kwa uhakika ni hatua stahiki namna gani inaweza kuchukuliwa…” Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Nguvu za Wanaume kuwatesa wanawake



1.       Mwanaume ana nguvu ya kumpenda mwanamke katika njia yoyote ambayo hajawahi kupendwa na lakini kumuumiza katika njia ile ile


2.       Mwanaume ana nguvu kumjali mwanamke kama marikia kisha kumgeuza nyuma na kumfanya ajihisi kama angekua hajazaliwa
3.       Mwanaume ana nguvu ya kumfanya mwanamke akalia kwa furaha na pia kumgeuza nyuma na kumfanya akalia kwa maumivu na hasira
4.       Mwanaume ananguvu ya kumfanya mwanamke kujiona huru na pia kumfanya kuchukia na kujiona asiye faa.
5.       Mwanaume ananguvu ya kumwangalia mwamke usoni na kumwambia anampenda lakini wakati huo huo anageuka na kulala na rafiki wa karibu wa mwanamke huyo
6.       Mwanaume ananguvu yakumfanya mwanamke akampenda ndani ya siku moja na kumfanya mwanamke amchukie ndani ya dakika moja

Kwa nini wanaume wananguvu hizo?
1.       Wananguvu nyingi kwasababu tunawapa nguvu hizo Mfano: Asilimia kubwa ya wanawake wanapoingia kwenye mahusiano huwaza mbali (Kuoana) Lakini wanaume wao hujaribu tu.
2.       Nguvu za mwanaume si chochote bila mwanamke ingawa wengi wao hujiona wao wako sahihi kuliko.
3.       Kwahiyo ndugu zangu kama unawakati mgumu kati yako na mwanaume wako na umetambua anakutendea vibaya kumbuka kuwa anafanya kile ambacho umekiruhusu

Lakini katika yote tunatakiwa kukumbuka tu Mwenyezi Mungu ameshatuandalia watu sahihi wakuishi nao hivyo tunatakiwa kuwa makini na kujipa moyo kwani mtu sahihi yupo na huja kwa wakati. Hakuna kuumia sana katika hili tunachotakiwa kufanya ni kuyakabidhi mahusiano yetu kwa Mungu.