Tuesday, May 20, 2014

Hatimaye Msanii Adam Philip azikwa leo katika viwanja vya Kinondoni.


Mwingizaji huyu mwenye umri wa miaka 38 alifariki ghafla kwenye kambi ya kurekodi filamu na wasanii wenzake iliyopo katika Nyumba ya Kulala Wageni ya Silvarado iliyopo Sinza ya Kwaremmy, Dar.Kifo chake kilitokea  akiwa njiani kukimbizwa kwenye Hospitali ya Mama Ngoma, Mwenge jijini Dar es Salaam baada ya kuugua. 

 Marehemu Adamu Enzi za uhai wake


Chanzo cha kifo chake inasemekana ni vidonda vya tumbo ambao msanii wa Bongo Fleva, Aboubakar Katwila ‘Q-Chillah’ alisema muda mchache kabla ya kufikwa na mauti,  Kuambiana alimlalamikia maumivu ya tumbo ambapo Ijumaa iliyopita alisema hali yake si nzuri kwani alikuwa akiendesha damu tupu.
Gari lililo beba mwili wa Marehemu kuelekea nyumbani kwake Bunju

Waombolezaji wakilia kwa majonzi


 Mwili wa Marehemu ukitolewa kuajili ya kupelekwa Leaders kuajili ya kuaga

 Baadhi ya wasanii wakiomboleza


Wasanii wameubeba mwili wa Marehe

 Wakijiandaa kuupokea mwili wa marehem

Mwili ukitolewa kwenye gari



Msanii Steve akilia kwa kuondokewa na mpendwa wao


Hivyo ndivyo Adam Philip alivyo tutoka. Tulikupenda lakini Mungu amekupenda zaindi. Mwenyezi Mungu aiweke roho ya marehemu mahara pema Amina.





Saturday, May 10, 2014

RAY C ASIMULIA ALIVYOKICHUNGULIA KIFO


Stori: MUSA MATEJA

MUNGU mkubwa! Staa wa muziki wa Kizazi Kipya Bongo, Rehema Chalamila ‘Ray C’, amesimulia jinsi alivyochungulia kifo baada ya kutikiswa na ugonjwa hatari na tishio ulioibuka hivi karibuni wa Homa ya Dengue.
Staa wa muziki wa Kizazi Kipya Bongo, Rehema Chalamila ‘Ray C’, akiwa kwenye red carpet ya Kilimanjaro Tanzania Music Awards.
Akifunguka mbele ya gazeti hili juzi baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini Mwananyamala, Dar alikokuwa amelazwa, Ray C au Kiuno Bila Mfupa alisema kwamba kwenye…
Stori: MUSA MATEJA
MUNGU mkubwa! Staa wa muziki wa Kizazi Kipya Bongo, Rehema Chalamila ‘Ray C’, amesimulia jinsi alivyochungulia kifo baada ya kutikiswa na ugonjwa hatari na tishio ulioibuka hivi karibuni wa Homa ya Dengue.
Staa wa muziki wa Kizazi Kipya Bongo, Rehema Chalamila ‘Ray C’, akiwa kwenye red carpet ya Kilimanjaro Tanzania Music Awards.
Akifunguka mbele ya gazeti hili juzi baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini Mwananyamala, Dar alikokuwa amelazwa, Ray C au Kiuno Bila Mfupa alisema kwamba kwenye maisha yake hajawahi kushikwa na ugonjwa wenye mateso makali, tena ya muda mfupi kama ilivyokuwa juzikati alipopata ugonjwa huo.
Alisema kwamba dakika chache tu baada ya kuamka kitandani alikuwa akijisikia kichwa kikiuma kama kinataka kuchomoka ambapo bila kuremba aliwasha gari lake na kukimbilia Hospitali ya Mwananyamala.
Staa huyo wa Ngoma ya Na Wewe Milele alisema alipofika kwa kudra za muumba alilazwa tayari kwa kutundikwa dripu.
“Huwezi kuamini baada ya madaktari kunipima na kugundua nina Ugonjwa wa Dengue, walinishangaa sana hata namna nilipofika pale na kwamba sikutumia dawa yoyote ya kutuliza maumivu kwa sababu maumivu yake huwa ni lazima utatafuta tu dawa ya kukufanya upoze maumivu.
“Madaktari wengine wakatishika zaidi maana walisema kama ukimeza vidonge vya ‘Diclopa’ unaweza kupoteza maisha mara moja.
“Katika magonjwa ya ajabu na yanayostahili kutafutiwa kinga mara moja basi huu ni ugonjwa wa kwanza ambao serikali inatakiwa iwe macho sana maana haufai hata kidogo.
“Tena unatisha sana na wasipoangalia utapoteza maisha ya Watanzania kibao kama hawatautafutia kinga au kuwapa Watanzania elimu ya kutosha.
“Mateso niliyoyapata kwa siku mbili nilizolazwa Mwananyamala ni elimu tosha kabisa na kwamba ningekuwa na uwezo wa kuzunguka au kupata nafasi ya kuongea na wakuu wa nchi basi mara moja ningewaomba wafanye jitihada za haraka kuhakikisha wanapata chanjo kwa ajili ya kuudhibiti mfumko wa gonjwa hilo.
“Dengue unaambukizwa na mbu tena wa mchana na dawa yake ni panadol tu!” alimalizia Ray C.

Soma Hapa magazeti ya Ijumaa ya leo tarehe 9 May, 2014. WEMA ANASA USHAHIDI KAJALA KUMUIBIA BWANA




Stori: IMELDA MTEMA

Unaweza ukaficha siri na ukaamini hakuna atakayejua bila kukumbuka kuwa hakuna siri ya watu wawili! Hatimaye Wema Isaac Sepetu amenasa ushahidi wa aliyekuwa rafikiye kipenzi, Kajala Masanja wa kumwibia aliyekuwa bwana’ke, Clement au CK, yule kigogo wa ikulu.
Wema Sepetu.
MIL. 13 KISINGIZIO TU

Habari za mjini kwa wiki nzima ni kusambaa kwa ujumbe mfupi (SMS) za kimapenzi za Kajala na CK ambazo sasa zimefunua kisa kamili cha mastaa hao kuhitilafiana huku Sh. Milioni 13 zikiwa…
Stori: IMELDA MTEMA
Unaweza ukaficha siri na ukaamini hakuna atakayejua bila kukumbuka kuwa hakuna siri ya watu wawili! Hatimaye Wema Isaac Sepetu amenasa ushahidi wa aliyekuwa rafikiye kipenzi, Kajala Masanja wa kumwibia aliyekuwa bwana’ke, Clement au CK, yule kigogo wa ikulu.
Wema Sepetu.
MIL. 13 KISINGIZIO TU
Habari za mjini kwa wiki nzima ni kusambaa kwa ujumbe mfupi (SMS) za kimapenzi za Kajala na CK ambazo sasa zimefunua kisa kamili cha mastaa hao kuhitilafiana huku Sh. Milioni 13 zikiwa kisingizio tu.
WEMA ALIKUWA ANATAFUTA USHAHIDI?
Kwa mujibu wa chanzo makini kilicho karibu na mastaa hao, kupatikana kwa meseji hizo ni kama mpango wa Mungu, kwani sasa kitendawili kimeteguka.
Baadhi ya meseji zilizonaswa.
“Wema alikuwa anatafuta ushahidi kama kweli Kajala anatembea na CK hivyo sasa amepata ushahidi.
“Mwenye macho haambiwi tazama na kama hujui kusoma hata picha huoni? Ama kweli kikulacho ki nguoni mwako!” Kilisema chanzo hicho.
Habari za ndani zilieleza kuwa meseji hizo zilikutwa kwenye simu ya CK na mwanamke mwingine ambaye naye anadaiwa kutoka na kigogo huyo, aliyetajwa kwa jina moja la Naima aliyekwenda kumbwagia ‘zigo’ Wema kwa ajili ya ushahidi.
Kajala Masanja.
Ilisemekana kwamba Naima alimuomba simu CK kwa kuwa ya kwake ilikuwa mbovu.
Habari zilizidi kudai kuwa baada ya CK kumpa mpenzi wake huyo simu yake, kumbe zile meseji alizokuwa akichati na Kajala alikuwa amesahau kuzifuta ndipo zilipobambwa.
Mpashaji wetu aliweka wazi kwamba meseji zile zilimshangaza Naima kwa kuwa yeye alikuwa ni mmoja wa watu ambao walikuwa hawaamini kabisa kama kulikuwa na ukweli wowote kuhusu tuhuma za Kajala kutembea na CK.
NAIMA ACHANGANYIKIWA
“Yaani Naima alipoziona meseji alichanganyikiwa kabisa, alikuwa kama kachomwa sindano ya ganzi kwani alikuwa ni mmoja wa watu ambao  hawaamini kabisa kama kweli Kajala anatembea na CK.
“Naima alipokaa vizuri ndipo akaanzisha timbwili lenye ujazo mkubwa na CK,” kilisema chanzo hicho.
Mnyetishaji wetu aliendelea kutiririka kuwa katika SMS hizo ambazo zilionesha waziwazi namba ya Kajala, zilikuwa zikielezea namna CK alivyokuwa akimuomba msamaha Kajala kwa kutopokea simu yake.

Kajala na Wema wakati wa ushosti wao.
HUU HAPA MZIGO
Mtiririko na meseji hizo ulikuwa hivi;
CK: “Mama mimi sipendi kukatiwa simu  pze, ok sawa lakini mi nakupenda.
Kajala: Kwa hiyo ndiyo unaniambiaje?
CK: Umeamua kuniblock?
CK: Kwa nini hupokei simu zangu?
CK: Unaponikatia simu wakati mimi naongea sijapenda sijui nijielezeje mama haya sawa.
Kajala: Fanya mambo.
MZIGO MIKONONI MWA ‘MNYAMWEZI’ WEMA
Ilisemekana kwamba baada ya Naima kuona meseji hizo alizihifadhi ili akamfikishie Wema ‘Myamwezi’ na kumuonesha jinsi rafiki yake alivyokuwa siyo mwaminfu kwake kitu ambacho alikifanikisha.
Habari zilidai kuwa baada ya Wema kuona SMS hizo alipatwa na mshtuko mkubwa kwani alikuwa haamini kama ni jambo analoweza kulifanya rafiki yake Kajala.
Ujumbe mwingine ulionaswa.
BOFYA HAPA KUMSIKIA ‘MADAM’
Baada ya ishu hiyo kuwa ndiyo habari ya mjini, gazeti hili lilijiongeza ambapo lilimsaka Wema ili kuzungumzia kuhusu meseji hizo.
Alipopatikana, Wema alifunguka kuwa  amesikitishwa mno na kitendo cha Kajala.
Wema alisema bora angefanya mtu mwingine yeyote lakini siyo Kajala aliyejitolea kuyaokoa maisha yake.
“Ukweli kabisa angefanya mtu mwingine yeyote wala isingekuwa ishu lakini siyo K. Aisee K amenishangaza na kuniumiza mno.
“Nilikuwa nimeshapanga niweke naye mambo sawa maisha yaendelee kama zamani lakini kwa hili siwezi kumsamehe tena,” alisema Wema aliyeonekana kukerwa na kucharuka vibaya.
HUYU HAPA MAMA WEMA
Baada ya kumalizana na Wema, gazeti hili lilimtafuta mama Wema, Mariam Sepetu ili kuzungumzia jambo hilo ambapo alisema kuwa siku zote alimwambia mwanaye kuwa achague marafiki wa kuwa nao lakini hakulitilia maanani.
“Unajua nilikuwa namwambia Wema kila siku, achague marafiki ambao atakuwa nao. Wengine siyo marafiki wa kweli, ndiyo kama hivyo ilivyotokea, nawaachia wenyewe mimi sina la kusema,” alisema mama Wema.
KAJALA VIPI?
Hata hivyo, gazeti lilimtafuta Kajala kwa njia mbalimbali lakini lilitonywa kuwa yupo China kwa ‘biashara zake’.
Katika mahojiano maalum na gazeti pacha la hili, Ijumaa Wikienda hivi karibuni, Kajala alikana kuwa hata na namba ya CK.
“Katika maisha yangu CK niliwahi kuonana naye mara moja tu, sina hata namba yake ya simu,” alinukuliwa Kajala.
TEAM WEMA YASHANGILIA USHINDI
Kwa upande wake lile kundi linalojiita Team Wema katika mitandao ya kijamii ilijipongeza kwa kupata ushahidi huo ambao sasa umeleta sura mpya ya ugomvi wa wawili hao.
Sehemu ya maoni mengi mitandaoni ilisomeka: “Sasa kule kulia kote runingani na mwanaye matokeo yake ndiyo haya? Kama kweli Kajala kamfanyia Wema hivyo, basi anapaswa kuomba msamaha hata kama Wema yupo na mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.