Tuesday, March 18, 2014

Dawa ya kuondoa Mistari, Michirizi, Mipasuko (Strech Marks) mwilini


 

Ukiangalia picha hizi utaelewa nazungumzia nini au namaanisha nini? 
ALAMA ZA MICHIRIZI KWENYE PAJA

Kabla hatujaangalia namna alama hizi zinavyotokea, tukumbushane sehemu muhimu za ngozi. Ngozi imegawanyika katika sehemu kuu tatu, sehemu ya nje (Epidermis), sehemu ya kati (Dermis) na sehemu ya ndani (Hypodermis).
Alama hutokea baada ya sehemu ya kati ya ngozi, dermis, kutanuka ghafla ndani ya muda mfupi kutokana na vitu kama mazoezi makali (kunyanyua vitu vizito), mtu kuongezeka uzito ghafla au obesity, pia kuna baadhi ya dawa au homoni (Glucocorticoids), ambazo kwa namna moja au nyingine huathiri tishu za kwenye ngozi na hivyo kupelekea mtu akapata alama za michirizi. Ujauzito kwa baadhi ya wanawake na pia mambo ya kurithi yameonekana kuchangia mtu kupata alama hizi katika ngozi yake.

Michirizi, mipasuko, mistari au kwa kitaalum Strech marks
inasababishwa na vitu vifuatavyo:-
- Ujauzito
- Kuongezeka kwa mwili (unene)
- Ukuaji wa haraka wakati wa kubalehe
- Mabadiliko ya mwili

Mpenzi msomaji, kwa kawaida michirizi hii huwa haimletei mtu maumivu ya aina yoyote, bali jambo kubwa huwa ni kuubadili muonekano wa ngozi ya mtu. Kwa baadhi ya watu michirizi hii huwa ni mikubwa sana, na kwa namna moja au nyingine humnyima mtu uhuru au humfanya mtu asiwe na amani pindi anapokuwa mbele za watu kwa kutegemeana na michirizi hiyo imetokea sehemu gani ya mwili.


Lakini hii hali inaweza kupotea kabisa iwapo utafanya mambo yafuatayo:-
1. Upakaji wa mafuta laini (Lotion) aina ya
Vaseline Intensive care tumboni katika kipindi chote cha
ujauzito kinasaidia kutopata tatizo hili.

2. Upakaji wa srub ya Apricot ni dawa ya haraka ya tatizo hili

3. Upakaji wa Mafuta ya Lavender mara 2 kwa siku yanaondoa
tatizo hili kwa muda mfupi sana
4. Mchanganyiko huu ni dawa nzuri na ya kuaminika,
ni vizuri ukihifadhi mchanganyiko wako ndani
ya Friji kwa kipindi chote cha matumizi.

- 1/2 kikombe cha olive oil
- 1/4 kikombe cha alove vera gel
- Majimaji ya vidonge 6 vya vitamini E
- Majimaji ya Vidonge 4 vya Vitamini A

No comments:

Post a Comment