Thursday, October 3, 2013

JINSI YA KUPIKA PILAU LA NYAMA YA NG'OMBE

Leo nataka niwape somo la upishi wa Pilau. Jamani mchele ni mmoja lakini mapishi ni mbalimbali wapo watakao loweka wapo watao kaanga lakini mwisho tunapata chakula ki 1. Leo nitaongelea kidogo kuhusu Pilau.

Pilau ni Chakula kitam sana na chenye mvuto wa mwonekano wake hasa kikipabwa kwa vitu tofauti tofauti. Kama Karoti, Hoho, Njegere na hata Nyanya pia.
 Leo tutapika Pilau la Nyama ya Ngombe kwanza unatakiwa kuandaa vitu vifuatavyo.

MAHITAJI
Mchele (Basmati) 3 vikombe 

                             
Nyama ya ngo’mbe 1 kg
                       
Pilipili boga  1 kubwa
                                
Nyanya  2 kubwa
                         
Vitunguu maji 2 vikubwa
                       
Tangawizi 1 kijiko cha chai
                          
Ndimu1




                               







Mafuta ya kupikia  ½ kikombe
                  
Mdalasini   ½  kijiko cha chai
             


















Binzari nyembamba 1 kijiko cha chai
                           
Pilipili manga   ½ Kijiko cha chai
Hiliki  ½ Kijiko cha chai
                        

                                 

                                
     
             
                              




Hatua:
  • Chemsha nyama yako mpaka iive, uwe umeweka chumvi kiasi, hakikisha nyama ina supu ya kutosha wakati wa kuichemsha
  • Osha mchele wako tayari kwa kuutumia na kisha utenge pembeni
  • Weka sufuria jikoni, kisha ongeza mafuta. Yakisha pata moto weka vitunguu maji vilivyokatwakatwa na kuaanga viive. Ongeza chumvi kiasi na endelea kukoroga
  • Ongeza vitunguu swaumu vilivyopondwa na endelea kukoroga, koroga mpaka vitunguu vigeuke kuwa rangi ya kahawia na kuiva
  • Ongeza viazi ulaya, vilivyomenywa na kukatwakatwa kwa ukubwa uupendao, endelea kukoroga ili vipate kuiva


  • Ongeza njegere na endelea kukoroga ili vipate kuiva




  • Weka vipande vya nyama iliyochemka vyema ndani ya mchanganyiko wako. Koroga mchanganyiko huo na acha kwa dakika chache uive vyema




  • Na hivi ndo itakavoonekana baada ya dakika kama 10 hivi ulizoacha mchanganyiko uive vyema 






  • Sasa ndo tunaanza kuweka viungo vya pilau na tunaanza na vile ambavyo havijatwangwa. Anza na iliki na Mdalasini huku unaongeza maji pale yanapokauka





  • Ongeza viungo vingine naongelea  weka binzari nyembamba pia na koroga ili vichanganyike vyema. Lazma harufu nzuri utaisikia maana mchanganyiko wa viungo hivi una harufu tamu mnoo 

  • .




      
    • Supu uliyochemshia nyama itakua inaonekana hivi baada ya kuondoa nyama. Yaonekana tamu kunyweka ila usiinywe inahusika sana kwenye pishi letu 
    • Weka mchele wako uliokwisha kuuosha jikoni kisha endelea kuchanganya ili viungo vichanganyike vyema

                                        


    • Weka supu ya ya nyama kisha endelea kuchanganya

                                 


    • Weka viungo vya unga na Endelea kuchanganya kwa mda kidogo ili mchanyanyiko wa viungo uchanganyikane vizuri







  • Acha mchanganyiko uweze kuchanganyiko vyema huku vikichemka kwa dakika kadhaa na hivi ndo itakavoonekana





    • Funika Chakula chako kwa daki kadhaa ili kichemke vyema










  • Baada ya dakika kama 5 angalia chakula chako, kumbuka kupunguza moto pale maji yanapoanza kukauka. Angalia wali kama umeanza kuiva na kama bado haujaiva na maji yamepungua basi ongeza maji huku unaacha viweze kuiva vyema






  • Hivi ndio itakavyoonekana pale pilau yako itakapoanza kuiva vyema. endelea kupunguza moto kwani tayari menyu inakaribia kuiva




  • Maji yakisha kauka geuza chakula ili kichanganyikane vizuri tayari kwa kupakua
                                           

    Pakua chakula kwenye chombo kwa aajili ya kuandaa mezani
                                                  
    Unaweza kupamba chakula chako kwa vitu tofauti ulivyo andaa kama vile Nyanya, Hoho, Mbogamboga au Karoti.

    Chakula tayari kwa kuliwa











                                                   

    10 comments:

    1. pilau nzuri ila hukusema nyanya unaweka wakati gani na hoho

      ReplyDelete
      Replies
      1. Soma vizuri bwana nimeelekeza sema hoho unaweza hata kusubiri mwishon kwa wale wasiopenda ilainike na wanapenda kusikia harufu yake na kuona ukijani unawza hata kuiweka badae sana itabaki juu ili ibaki na rangi yake na harufu yake nzur

        Delete
    2. Nashkuru sana kwa msaada wako. Nimepata 'idea ya kupika pilau kwa ajili ya week end hii, pia nijumuike na family. Mwenyeezi mungu akulipe kwa hilo.

      ReplyDelete
      Replies
      1. Ahsante pia kwa kusoma mama Abdulrahman Endelea kusoma na kutoa maoni pale inapobid ahsante sana

        Delete
    3. kizito unasema pilau nzuri sana kama umesaionja vile,

      ReplyDelete
    4. Tunajifunza mengi..Mungu akulipe

      ReplyDelete
    5. Shukran sana. Nimefuata haya maagizo na ukweli ni kwamba, nimetengeneza Pilau tamu sana. Mungu akubariki na uendelee kutupa 'recipe' zingine kama hizi. Baraka tele.

      ReplyDelete
    6. hahaha pia mimi sikuona mahali nyanya na hoho huekewa but i now know where to start

      ReplyDelete