Friday, August 29, 2014

Patrick Ole Sosopi Mgombea wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa BAVICHA (Baraza la Vijana Chadema) awaomba watu wampigie kura

Patrick Ole Sosopi ni mgombea wa nafasi ya umakamu mwenyekiti wa BAVICHA (Baraza la Vijana Chadema). Historia yake ya uongozi na uadilifu wake umekuwa hauna shaka katika vipindi mbalimbali vya maisha yake. Historia yake ya uongozi ni kuanzia akiwa Elimu ya Sekondari mpaka Chuo Kikuu.

Patrick Ole Sosopi. Ni mmasai aliyezaliwa na kukulia mkoa Iringa, jimbo la Ismani. Ana umri wa miaka 28. Ni msomi wa shahada ya kwanza ya Biashara na utawala (rasilimali watu) kutoka chuo kikuu cha Ruaha (RUCO). 

Ni mpenda maendeleo na amekua mstari wa mbele kutetea ukombozi wa Taifa letu. Akielezea historia yake kwa ufupi Alijiunga rasmi na CHADEMA mwaka 2009 alipokuwa mwanafunzi wa mwaka wa kwanza akiamini ni chama pekee ambacho kina tija ya kuboresha maisha ya jamii yake ya kimasai na watu wote kwa ujumla na changamoto mbalimbali ambazo zilikuwa zikiwakabili.


Patrick Ole Sosopi ni mojawapo wa waanzilishi wa Chadema Students Organizati (CHASO) mkoani Iringa,  Ameshiriki katika mchakato wa ujenzi wa chama kwenye wilaya zote za mkoa wa Iringa pamoja na Mbeya. Aliaminiwa na vijana wa Ismani na kupata kura zote bila kupingwa na kuwa Mwenyekiti wa BAVICHA jimbo la Ismani. Baada ya kushauriwa na kushauriana na familia yake na vijana mbambali kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania, ameona agombee nafasi ya Umakamu Mwenyekiti wa BAVICHA Bara. Hivyo anaomba kula zako wewe Mtanzania ili kuleta mabadiliko na maendeleo katika nchi yetu. Uchaguzi unategemewa kufanyika tarehe 10/9/2014 Dar es salaam Makao makuu ya Chama.



 Partick Ole Sosopi akihutubia Wananchi wa Iringa Mjini




 Alipokuwa kwenye uchaguzi wa Kalenga Mwanzoni mwa mwaka huu

 Akihutubia wananchi wa Wilaya ya Kilolo
 Akiwa katika Jimbo lake la Isamani kama Mwenyekiti wa BAVICHA Jimbo hilo.


 Akiwa Pawaga na wadau wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)

 

No comments:

Post a Comment