Thursday, November 27, 2014

Nguvu za Wanaume kuwatesa wanawake



1.       Mwanaume ana nguvu ya kumpenda mwanamke katika njia yoyote ambayo hajawahi kupendwa na lakini kumuumiza katika njia ile ile


2.       Mwanaume ana nguvu kumjali mwanamke kama marikia kisha kumgeuza nyuma na kumfanya ajihisi kama angekua hajazaliwa
3.       Mwanaume ana nguvu ya kumfanya mwanamke akalia kwa furaha na pia kumgeuza nyuma na kumfanya akalia kwa maumivu na hasira
4.       Mwanaume ananguvu ya kumfanya mwanamke kujiona huru na pia kumfanya kuchukia na kujiona asiye faa.
5.       Mwanaume ananguvu ya kumwangalia mwamke usoni na kumwambia anampenda lakini wakati huo huo anageuka na kulala na rafiki wa karibu wa mwanamke huyo
6.       Mwanaume ananguvu yakumfanya mwanamke akampenda ndani ya siku moja na kumfanya mwanamke amchukie ndani ya dakika moja

Kwa nini wanaume wananguvu hizo?
1.       Wananguvu nyingi kwasababu tunawapa nguvu hizo Mfano: Asilimia kubwa ya wanawake wanapoingia kwenye mahusiano huwaza mbali (Kuoana) Lakini wanaume wao hujaribu tu.
2.       Nguvu za mwanaume si chochote bila mwanamke ingawa wengi wao hujiona wao wako sahihi kuliko.
3.       Kwahiyo ndugu zangu kama unawakati mgumu kati yako na mwanaume wako na umetambua anakutendea vibaya kumbuka kuwa anafanya kile ambacho umekiruhusu

Lakini katika yote tunatakiwa kukumbuka tu Mwenyezi Mungu ameshatuandalia watu sahihi wakuishi nao hivyo tunatakiwa kuwa makini na kujipa moyo kwani mtu sahihi yupo na huja kwa wakati. Hakuna kuumia sana katika hili tunachotakiwa kufanya ni kuyakabidhi mahusiano yetu kwa Mungu.

No comments:

Post a Comment