Sunday, March 16, 2014

Crimea yapiga kura kuamua iwapo jimbo hilo libaki Ukraine au lijiunge na Urusi


Wacrimea wakipiga kura ya maoniInaarifiwa kuwa upigaji kura unaendelea haraka Crimea katika kura ya maoni ya kuamua iwapo jimbo hilo libaki Ukraine au lijiunge na Urusi. Waandishi wa habari wanasema kuna kama sherehe wakati wa kupiga kura, huku bendera za Urusi na Crimea zikipepea na watu wanatakiana "siku njema ya kupiga kura'. Lakini piya kuna Wacrimea - pamoja na wale wa kabila la Tartar ambao ni asili-mia-12 ya watu wa Crimea - hao wanasusia kura. Huku nyuma kaimu waziri wa ulinzi wa Ukraine amesema Urusi imekubali kuacha kuzingira makambi ya jeshi la Ukraine huko Crimea hadi Ijumaa, ambapo bunge la Urusi litaanza kujadili sheria ya kuungana na maeneo mapya.
Chanzo BBC Swahili

No comments:

Post a Comment