Tuesday, January 6, 2015
Mayness Emmanuel Chapote Blog: Ahsante sana wadau wangu mnao shiriki nami kikamil...
Mayness Emmanuel Chapote Blog: Ahsante sana wadau wangu mnao shiriki nami kikamil...: Ninamshukuru sana mwenyezi Mungu kwa ulizi wake Mkuu kwangu amenilinda mwaka Mzima uliopita 2014 mpaka sasa 2015. Ahsante sana w...
Saturday, January 3, 2015
URAIS 2015: NYALANDU AKESHA AKICHEZA SEBENE!
WAZIRI wa Mali Asili na Utalii, Lazaro Nyalandu ambaye ametangaza nia ya kuwania urais wa nchi amefanya kufuru kubwa katika Kanisa la Efatha linaloongozwa na Nabii Josephat Mwingira, mjini Kibaha, Pwani baada ya kusakata sebene la Injili usiku wa manane.
WAZIRI wa Mali Asili na Utalii, Lazaro Nyalandu ambaye ametangaza nia ya kuwania urais wa nchi amefanya kufuru kubwa katika Kanisa la Efatha linaloongozwa na Nabii Josephat Mwingira, mjini Kibaha, Pwani baada ya kusakata sebene la Injili usiku wa manane.
Kuonesha msisitizo, Nabii Mwingira naye aliingilia jukwaani na kucheza muziki huo wa Injili huku akighani maneno ya Mungu kwa kutumia kipaza sauti alichokuwa nacho mkononi saa zote za hafla hiyo.
Mara baada ya saa sita na dakika 35 usiku kutimia Nyalandu ambaye alikuwa mgeni rasmi alikaribishwa kusema neno ambapo alipanda jukwaani na kumshukuru Mungu kwa kuuona mwaka mpya 2015.
Hata hivyo, alijipigia kampeni kwa kuwakumbusha waumini hao kuwa Oktoba mwaka huu Tanzania itakuwa na tukio kubwa, hivyo waumini hao kwake ni muhimu kwani wakati ukifika atawaomba kura zao.
“Wakati nacheza pale nimewaona wanakwaya na kuhisi kwamba wana kitu moyoni. Nawaambia Oktoba ikifika lazima mchague vijana nami nitawahitaji sana kuja kuniimbia,” alisema.
“Huwa sisi hatuamini katika mashetani, tunaamini katika roho saba... hivyo natamka kwamba wote waliopo hapa na wana nia zao katika vifua vyao, basi Mungu atawapa,” alisema Mwingira huku akishangiliwa.
Hii ni mara ya pili kwa Nyalandu kujipigia kampeni za urais kanisani, mara ya kwanza ni hivi karibuni katika jimbo lake alipokwenda katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania kijijini Ilongelo, Singida.
Kiongozi huyo pia alikwenda katika Shule ya Msikiti wa Ilongelo ambapo inadaiwa alitoa msaada wa kusaidia shule na kanisa hilo.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Taifa wa CCM, Nape Nnauye hakupatikana ili aweze kutoa maoni yake kuhusu vitendo hivyo kwani simu yake ilikuwa haipatikani.
Baadhi ya wagombea waliotangaza nia kutoka CCM ni Dk Hamisi Kigwangalla, Januari Makamba, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na wengine wanaotajwatajwa ni Steven Wassira, Bernard Membe, Samwel Sitta na Edward Lowassa.
NINGEKUWA MIMI NYALANDU, NISINGETANGAZA KUGOMBEA URAIS
Kwako Waziri wa Maliasili na Utalii na Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Samuel Nyalandu.
Najua uko bize sana kwa sasa ukiweka sawa mipango yako kuhakikisha mwaka huu unaingia ikulu katika uchaguzi mkuu ujao, najua itakuwa vigumu kwa ‘kapuku’ kama mimi kuonana na wewe ndiyo maana nimeamua kutumia ukurasa huu kufikisha ujumbe wangu kwako.
Najua uko bize sana kwa sasa ukiweka sawa mipango yako kuhakikisha mwaka huu unaingia ikulu katika uchaguzi mkuu ujao, najua itakuwa vigumu kwa ‘kapuku’ kama mimi kuonana na wewe ndiyo maana nimeamua kutumia ukurasa huu kufikisha ujumbe wangu kwako.
Mheshimiwa, mimi sikuzaliwa Agosti 18, 1970 kama wewe wala sijawahi
kusoma Shule ya Msingi Pohama, Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Kibaha
wala sijawahi kusoma Shule ya Sekondari ya Illboru na kuhitimu kidato
cha sita kama wewe.
Sijawahi kusoma vyuo mbalimbali…
Kwako Waziri wa Maliasili na Utalii na Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Samuel Nyalandu.
Najua uko bize sana kwa sasa ukiweka sawa mipango yako kuhakikisha mwaka huu unaingia ikulu katika uchaguzi mkuu ujao, najua itakuwa vigumu kwa ‘kapuku’ kama mimi kuonana na wewe ndiyo maana nimeamua kutumia ukurasa huu kufikisha ujumbe wangu kwako.
Najua uko bize sana kwa sasa ukiweka sawa mipango yako kuhakikisha mwaka huu unaingia ikulu katika uchaguzi mkuu ujao, najua itakuwa vigumu kwa ‘kapuku’ kama mimi kuonana na wewe ndiyo maana nimeamua kutumia ukurasa huu kufikisha ujumbe wangu kwako.
Mheshimiwa, mimi sikuzaliwa Agosti 18, 1970 kama wewe wala sijawahi
kusoma Shule ya Msingi Pohama, Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Kibaha
wala sijawahi kusoma Shule ya Sekondari ya Illboru na kuhitimu kidato
cha sita kama wewe.
Sijawahi kusoma vyuo mbalimbali duniani kama University of Buckingham
cha Uingereza, Wartburg College na Waldorf College, vyote vya Marekani
kama wewe. Sijui chochote kuhusu uongozi wala siasa, niponipo tu, kapuku
nisiye na mbele wala nyuma.
Hata hivyo, ningekuwa mimi katika nafasi yako, walahi nakuapia
nisingepaza sauti yangu na kutangaza kwamba nataka kugombea urais kama
ulivyofanya wewe hivi karibuni Katika Uwanja wa Ilongero, kwenye jimbo
lako la Singida Kaskazini.
Najua ni haki yako ya msingi kugombea kama ilivyo kwa Mtanzania
mwingine yeyote lakini nakuhakikishia, kama ungepata nafasi ya
kujitathmini wewe kwanza, kuangalia udhaifu mkubwa uliouonesha tangu
ulipokuwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Naibu Waziri wa Maliasili
na Utalii hadi sasa ukiwa waziri kamili katika Wizara ya Maliasili na
Utalii, usingethubutu kutangaza nia.
Mheshimiwa, umesahau jinsi ulivyokumbwa na kashfa kibao za kudaiwa
kushirikiana na kampuni za kigeni za utalii na uwindaji kuihujumu
serikali kwa kujenga mazingira ya kukwepa kodi?
Umesahau jinsi ulivyohusishwa na kampuni ambayo inadaiwa una mgongano nayo wa kimaslahi ya Ahsante Tours, ikidaiwa ulishinikiza kampuni hiyo isamehewe mamilioni ya kodi mpaka TANAPA walipoikomalia ndiyo kodi ikalipwa?
Mheshimiwa, umesahau jinsi ulivyoidhinisha ununuzi wa helikopta
chakavu eti kwa ajili ya kukabiliana na ujangili, mwisho helikopta hiyo
ikaanguka na kusababisha vifo vya marubani wetu wanne hivi karibuni?
Mheshimiwa, umesahau jinsi nchi yetu ilivyoingia kwenye doa kubwa kufuatia ujangili wa kupindukia na biashara ya meno ya tembo ilivyoshamiri kwa sababu ya wewe na wenzako kushindwa kutimiza majukumu yenu kwa umakini?
Mheshimiwa, umesahau jinsi nchi yetu ilivyoingia kwenye doa kubwa kufuatia ujangili wa kupindukia na biashara ya meno ya tembo ilivyoshamiri kwa sababu ya wewe na wenzako kushindwa kutimiza majukumu yenu kwa umakini?
Vipi kuhusu marekebisho ya hovyo ya sheria ya uwindaji unayoshikia
bango kwamba kipindi cha uwindaji kiongezwe kutoka muda wa miezi sita
hadi tisa kwa manufaa ya wawindaji bila kujali uhifadhi na kuzaliana kwa
wanyama wetu?
Madudu ambayo kwa namna moja au nyingine umekuwa ukidaiwa kuhusika
nayo, ni mengi mno. Nikisema nitaje mojamoja, nitayajaza ukurasa mzima.
Hapana mheshimiwa, utendaji wako katika sehemu zote ulizopita, hauridhishi. Umekuwa ukionekana ‘mzigo’ kila unapopita achilia mbali jimboni kwako ambako kuna ahadi kibao ulizitoa wakati wa kampeni lakini mpaka sasa hujazitimiza.
Kama kuongoza jimbo lako la Singida Kaskazini na kuongoza wizara moja
tu kumekushinda, utaweza kuongoza nchi? Ikulu ni mahali patakatifu
mheshimiwa, waachie wenye uwezo watangaze nia ya kugombea lakini siyo
wewe.
Friday, January 2, 2015
Mkesha wa Mwaka Mpya: Kila kona Uchaguzi Mkuu
Makamu wa Rais Dk Mohamed Gharib Bilali akiwaongoza wakazi wa Dar es
Salaam kusherehekea Mwaka mpya katika Uwanja waTaifa, Dar es Salaam.
Kulia ni Mkuu wa Mkoa, Saidi Mecky Sadiki na kushoto ni Mwenyekiti wa
Kamati ya mkesha, Godfrey Mallase. Picha na Anthony Siame
Na Waandishi Wetu, Mwananchi
Kwa ufupi
Wakati viongozi wa dini wakijikita katika
kuhamasisha haki kutendekea katika uchaguzi na kuepuka vitendo
vinavyoweza kusababisha uvunjifu wa amani na Makamu wa Rais, Dk Mohamed
Ghalib Bilal aliwataka wananchi kuwatosa wagombea wote watakaotumia
rushwa kuwashawishi wawachague.
Dar es Salaam. Ujumbe mahususi wa jinsi ya
kushiriki na kuvuka salama katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba ulitawala
salamu za kuukaribisha mwaka 2015 zilizotolewa juzi na viongozi wa dini
na Serikali katika maeneo mbalimbali nchini.
Wakati viongozi wa dini wakijikita katika
kuhamasisha haki kutendekea katika uchaguzi na kuepuka vitendo
vinavyoweza kusababisha uvunjifu wa amani na Makamu wa Rais, Dk Mohamed
Ghalib Bilal aliwataka wananchi kuwatosa wagombea wote watakaotumia
rushwa kuwashawishi wawachague.
Salamu hizo zilianza kutolewa juzi wakati wa
mkesha na Serikali ilitahadharishwa kuzingatia haki, usawa na demokrasia
katika kusimamia uchaguzi huo ili kuepuka machafuko hasa katika kipindi
cha uchaguzi huo.
Gwajima aonya
Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Mchungaji
Kiongozi, Josephat Gwajima katika misa ya mkesha uliyofanyika katika
viwanja vya kanisa hilo, Kawe Dar es Salaam, alisema: “Ili nchi iendelee
kuwa na amani, Serikali ihakikishe kuwa jeshi halitumiki katika hatua
yoyote ile kuelekea uchaguzi mkuu.”
Pamoja na kauli hiyo inayolenga mpango wa Tume ya
Taifa ya Uchaguzi (NEC) wa kutaka kutumia wanajeshi katika uandikishaji
wapigakura, Gwajima alisema pia ili kulinda amani ya nchi matokeo ya
uchaguzi yatangazwe kwa wakati na pasiwepo na wizi wa kura.
Alisema matumizi ya jeshi katika maandalizi na
usimamizi wa uchaguzi ni mwanzo wa uandaaji wa mapinduzi kwa kuwa
kufanya hivyo ni sawa na kuwatamanisha na kuwaonyesha askari hao njia za
kuingia Ikulu.
“Tanzania ni nchi ya kidemokrasia, hakuna sababu
zozote za kulihusisha jeshi katika harakati za uchaguzi na uwezekano
ulio wazi ni kuwa mwitikio wa kujiandikisha unaweza usiwe mzuri kutokana
na hilo. Lakini pia kama kuna viongozi waandamizi ndani yake ambao
wanawaunga mkono baadhi ya wagombea wanaweza kutoa amri katika maeneo
yao ufanyike upendeleo,” alisema.
Alisema hakutakuwa na maombi yatakayokuwa na
msaada endapo matokeo ya uchaguzi hayatatangazwa kwa wakati kwa kuwa
wapigakura watakuwa na shauku ya kujua hatima ya wale waliowachagua.
Katika mkesha huo uliohudhuriwa pia na Katibu Mkuu
wa Chadema, Dk Willbrod Slaa, Gwajima aliwaeleza maelfu ya waumini
waliohudhuria kuwa mwaka huu ni muafaka kwa ajili ya kuwaondoa wezi wote
wa rasilimali za umma katika nafasi za uongozi ili Taifa linufaike na
rasilimali lilizojaliwa.
Dk Slaa anena
Akiwahutubia waumini hao zaidi ya 70,000, Dk Slaa
alieleza misingi muhimu itakayoifanya Tanzania isonge mbele huku kila
mwananchi akinufaika na maendeleo husika.
AUNT: MUME WANGU HAJUI KAMA NINA MIMBA
Stori:Musa mateja
Msanii wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel ‘Mama Kijacho’ amefunguka kuwa, licha ya ujauzito wake kuwa mkubwa, mume wake Sunday Demonte hana taarifa yoyote juu ya kitumbo hicho.Akipiga stori na paparazi wetu hivi karibuni, Aunt alisema maneno hayo yanaweza kuwashangaza watu lakini ndiyo ukweli wenyewe.
Msanii wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel ‘Mama Kijacho’.
Alidai kuwa yeye na mume wake huyo hawajaachana na hajapewa talaka
kama watu wanavyodai lakini hajui kwamba ni mama mtarajiwa na…Msanii wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel ‘Mama Kijacho’ amefunguka kuwa, licha ya ujauzito wake kuwa mkubwa, mume wake Sunday Demonte hana taarifa yoyote juu ya kitumbo hicho.Akipiga stori na paparazi wetu hivi karibuni, Aunt alisema maneno hayo yanaweza kuwashangaza watu lakini ndiyo ukweli wenyewe.
Msanii wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel ‘Mama Kijacho’.
Alidai kuwa yeye na mume wake huyo hawajaachana na hajapewa talaka
kama watu wanavyodai lakini hajui kwamba ni mama mtarajiwa na hata
akijua hawezi kumuacha.“Kiukweli mume wangu hajui kuwa nina ujauzito na hata akijua wala hawezi kuniacha, ananipenda sana. Sijaachana naye na wala sijapewa talaka, hayo yanayosemwa ni umbeya tu,” alidai Aunt.
JOKATE: DIAMOND HANA AKILI TIMAMU
Staa wa urembo, muziki, filamu na ujasiriamali Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ au ‘Jojo’ amemrushia maneno makali aliyewahi kuwa mpenzi wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kuwa hana akili timamu kufuatia maneno aliyotoa kuwa enzi za uhusiano wao, eti mwanadada huyo alikuwa akichenga kumzalia mtoto.
Staa wa urembo, muziki, filamu na ujasiriamali Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ au ‘Jojo’.
MAHOJIANOKatika mahojiano maalum ya hivi karibuni kupitia Kipindi cha Mtu Kati cha Runinga ya GlobalTV Online chenye makao yake makuu ndani ya Ofisi za Global Publishers zilizopo Bamaga-Mwenge, Dar, Diamond alitoa madai kuwa, amekuwa akihaha kupata mtoto.
Alisema kwamba, katika harakati zake hizo, warembo ambao alishatoka nao kimapenzi akiwemo Jokate walikuwa wakimchezea mchezo mchafu ili wasimzalie kwa kuwa alikuwa akiwaambia anahitaji mtoto kwa udi na uvumba.
MZOZO MKUBWA
Hata hivyo, madai hayo ya Diamond yalizua mzozo mkubwa kwenye mitandao ya kijamii huku warembo hao wakipigwa za uso hivyo kutafuta namna ya kujitetea.“Hao akina…(wanatajwa warembo wa Diamond) watakuwa wana matatizo ya uzazi siyo bure.
“Ndiyo maana Dangote (Diamond) ameona bora aende kwa Zari (msanii wa Uganda, Zarinah Hassan) ambaye tayari ana mwanga wa kuzaa (ana watoto watatu),” ilisomeka sehemu ya maoni juu ya madai hayo ya Diamond kwenye Mtandao wa Instagram.
SIKIA MADAI YA DIAMOND
Diamond alifunguka: “Jokate na Wema (Sepetu) nilitamani sana wanizalie lakini walikuwa wakichengachenga, mambo mengine ujue si ya kuzungumza lakini inauma.”
JOKATE AJIBU MAPIGO
Kufuatia tuhuma hizo nzito huku kukiwa na madai pia, kwamba Jokate aliwahi kupigwa mimba ‘akaipanchi’, mwanadada huyo alipotafutwa na mwandishi wetu kujibu ‘shitaka’ linalomkabili alianza kwa kumshangaa staa huyo wa Ngoma ya Ntampata Wapi inayokimbiza kwa sasa.
Jokate alisema anamshangaa Diamond kuyazungumza maneno hayo hadharani na inaonesha asivyokuwa na akili timamu au ambayo haijakomaa.
JOJO ASHUKA NA MISTARI
“Diamond atuache, kila siku anatuzungumzia, hana akili timamu.
“Inadhihirisha kweli hana akili kwa kuwa mtu mwenye akili zake timamu hawezi kwenda kwenye chombo cha habari na kueleza hayo aliyoyasema,” alisema Jokate akionesha kukasirishwa na maneno ya Diamond.
Ukiacha Jokate na Wema ambaye naye aliwekwa kwenye kapu moja la kuchenga kumzalia, hakutaka kumjibu Diamond kwa kuwa hataki malumbano au makuu na mtu.
PENNY ALISHAJIBU
Pia jamaa huyo alimzungumzia aliyekuwa mwandani wake mwingine, Penniel Mwingilwa ‘Penny’ kuwa yeye alitoa mimba zake mbili kwa visingio tofauti. Katika majibu yake kupitia gazeti tumbo moja na hili, Risasi Jumamosi, toleo la wiki iliyopita, Penny alisema kuwa Diamond awe mkweli na aseme tatizo lake kwani anavyojua yeye hana uwezo wa kumpa mwanamke mimba.
Thursday, January 1, 2015
Ahsante sana wadau wangu mnao shiriki nami kikamilifu kusoma na kutoa maoni na mapendekezo katika Blog yangu. Ninawatakia mafanikio katika mwaka huu 2015 Kipekee ......
Ninamshukuru sana mwenyezi Mungu kwa ulizi wake Mkuu kwangu amenilinda
mwaka Mzima uliopita 2014 mpaka sasa 2015. Ahsante sana wadau wangu mnao
shiriki nami kikamilifu kusoma na kutoa maoni na mapendekezo katika
Blog yangu. Ninajua kazi hii ni ngumu sana na ninakua nikipata wakati
mgumu kutokana na ugumu wa majukumu niliyonayo. Inanipelekea wakati
kutowapa taarifa mala kwa mala. Ninatamani kuwa nanyi kila siku lakini
kuna wakati nazidiwa ila muamini kitu kimoja kuwa ninawapenda sana wadau
wangu. Kipekee pia napenda kuishukuru sana Familia yangu kwa kunipa
moyo na kuniombea katika magumu yote ninayo yapitia. Leo ninapenda kuwapa zawadi ndogo picha zangu ili mpate fahari ya macho. Pia ninawaomba msisite kutoa maoni kwani maoni yenu ndo yananijenga kurekebisha pale ninapo kosea.
Happy new year 2015 ndugu zangu. Nawapenda saaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaana

Utulivu kidogo

Mapumziko kidogo

Na my dada

Baba na watoto.

Na rafiki yangu kipenzi

Nikiwa na My baba
Ki kwetu kwetu
Dadaz na Mtoto
Nikiwa na dadaz
Hapa ni Dodoma na Bibi na Babu.
Burudani Dar es salaam
Mapumziko Mbeya moja
Weekend
Ofisi za watu
Ibadani J2
Nawapenda sana nina waahidi kuwapa habari na taarifa moto moto katika mwaka huu mpya 2015.
Subscribe to:
Posts (Atom)






