Friday, January 2, 2015

Mkesha wa Mwaka Mpya: Kila kona Uchaguzi Mkuu



Makamu wa Rais Dk Mohamed Gharib Bilali akiwaongoza wakazi wa Dar es Salaam kusherehekea Mwaka mpya katika Uwanja waTaifa, Dar es Salaam. Kulia ni Mkuu wa Mkoa, Saidi Mecky Sadiki na kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya mkesha, Godfrey Mallase. Picha na Anthony Siame 
Na Waandishi Wetu, Mwananchi


Kwa ufupi
Wakati viongozi wa dini wakijikita katika kuhamasisha haki kutendekea katika uchaguzi na kuepuka vitendo vinavyoweza kusababisha uvunjifu wa amani na Makamu wa Rais, Dk Mohamed Ghalib Bilal aliwataka wananchi kuwatosa wagombea wote watakaotumia rushwa kuwashawishi wawachague.

Dar es Salaam. Ujumbe mahususi wa jinsi ya kushiriki na kuvuka salama katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba ulitawala salamu za kuukaribisha mwaka 2015 zilizotolewa juzi na viongozi wa dini na Serikali katika maeneo mbalimbali nchini.
Wakati viongozi wa dini wakijikita katika kuhamasisha haki kutendekea katika uchaguzi na kuepuka vitendo vinavyoweza kusababisha uvunjifu wa amani na Makamu wa Rais, Dk Mohamed Ghalib Bilal aliwataka wananchi kuwatosa wagombea wote watakaotumia rushwa kuwashawishi wawachague.
Salamu hizo zilianza kutolewa juzi wakati wa mkesha na Serikali ilitahadharishwa kuzingatia haki, usawa na demokrasia katika kusimamia uchaguzi huo ili kuepuka machafuko hasa katika kipindi cha uchaguzi huo.
Gwajima aonya
Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Mchungaji Kiongozi, Josephat Gwajima katika misa ya mkesha uliyofanyika katika viwanja vya kanisa hilo, Kawe Dar es Salaam, alisema: “Ili nchi iendelee kuwa na amani, Serikali ihakikishe kuwa jeshi halitumiki katika hatua yoyote ile kuelekea uchaguzi mkuu.”
Pamoja na kauli hiyo inayolenga mpango wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) wa kutaka kutumia wanajeshi katika uandikishaji wapigakura, Gwajima alisema pia ili kulinda amani ya nchi matokeo ya uchaguzi yatangazwe kwa wakati na pasiwepo na wizi wa kura.
Alisema matumizi ya jeshi katika maandalizi na usimamizi wa uchaguzi ni mwanzo wa uandaaji wa mapinduzi kwa kuwa kufanya hivyo ni sawa na kuwatamanisha na kuwaonyesha askari hao njia za kuingia Ikulu.
“Tanzania ni nchi ya kidemokrasia, hakuna sababu zozote za kulihusisha jeshi katika harakati za uchaguzi na uwezekano ulio wazi ni kuwa mwitikio wa kujiandikisha unaweza usiwe mzuri kutokana na hilo. Lakini pia kama kuna viongozi waandamizi ndani yake ambao wanawaunga mkono baadhi ya wagombea wanaweza kutoa amri katika maeneo yao ufanyike upendeleo,” alisema.
Alisema hakutakuwa na maombi yatakayokuwa na msaada endapo matokeo ya uchaguzi hayatatangazwa kwa wakati kwa kuwa wapigakura watakuwa na shauku ya kujua hatima ya wale waliowachagua.
Katika mkesha huo uliohudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbrod Slaa, Gwajima aliwaeleza maelfu ya waumini waliohudhuria kuwa mwaka huu ni muafaka kwa ajili ya kuwaondoa wezi wote wa rasilimali za umma katika nafasi za uongozi ili Taifa linufaike na rasilimali lilizojaliwa.
Dk Slaa anena
Akiwahutubia waumini hao zaidi ya 70,000, Dk Slaa alieleza misingi muhimu itakayoifanya Tanzania isonge mbele huku kila mwananchi akinufaika na maendeleo husika.

No comments:

Post a Comment