Friday, October 11, 2013

Ufisadi kwenye bajeti za shule

 
Ufisadi katika sekta ya elimu, ni tatizo sugu na bila shaka unahujumu hadhi ya elimu na uwepo wa shule na vyuo vikuu kote duniani . Hii ni kwa mujibu wa taarifa za ripoti ya kimataifa.
Shirika la kimataifa la Transparency International limechapisha utafiti unaoonyesha kuwa mwanafunzi mmoja katika kila wanafunzi sita, alilazimika kulipa rushwa ili apokee huduma za elimu.
Katika baadhi ya sehemu za Kusini mwa jangwa la Sahara na barani Asia, ufisadi unaowalazimisha wazazi kulipa kiwango kidogo cha pesa kwa nafasi ya shule ambayo alipaswa kuipata bila malipo.
Nako barani Ulaya hasa Mashariki mwa Ulaya, watu wanalazimika kulipa rushwa ili waweze kupata nafasi katika chuo kikuu.
Shirika hilo la mjini Berlin linalojulikana , kwa kuchunguza viwango vya pesa zinazotozwa kwa njia isiyo halali katika zaidi ya nchi 100, ilizingatia zaidi ya nyumba
114,000 kwa mahojiano.
Katika baadhi ya nchi ripoti hiyo inasema kuwa karibu thuluthi tatu ya watu nchini Cameroon na Urusi, wanaona mfumo wao wa elimu kama uliokumbwa na ufisadi si haba.

Hali halisi za shule barani Afrika
Nchini Urusi ufisadi umekithiri katika mfumo wake wa elimu
Madai ya ufisadi yalichocheza maandamano ya walimu nchini Brazil.
Matokeo ya utafiti yanaonyesha viwango vya juu sana vya rushwa katika sekta ya elimu.
Na nchini Pakistan, kulikuwa na onyo la maelfu ya shule hewa bila ya wanafunzi ingawa zilikuwa zinazopokea ufadhili wa kuwalipa walimu hewa.
Mapengo katika sekta ya elimu Kenya yalisababisha kupoteza kwa vitabu milioni 11. Nachini Tanzania , katika utafiti wa shule 180, iligunduliwa kuwa ufadhili haukuwafikia wanafunzi na shule husika.
Nchini Ugiriki, kulikuwa na tatizo la mapendeleo katika kutoa nafasi za kazi na watu kupandishwa cheo katika vyo vikuu.

Sasa kwa nini elimu ikumbwe na ufisadi hivi?

Wazazi wanawataka watoto wao wapate elimu nzuri na wanaweza kuhadaiwa na maafisa wanaodhibiti mifumo ya elimu hasa katika mataifa ya kiafrika ambako nafasi zaidi zinahitajika za watoto kusoma.

Nchini Nigeria dola milioni 21 zilipotea kwa miaka miwili
Pia yote haya yanahusu pesa nyingi za serikali zinazotolewa kwa shule za serikali. Nchini Nigeria ripoti hiyo imesema kuwa dola milioni 21 za kimarekani zilizonuiwa kwa matumizi ya shule, zilipotea kwa kipindi cha miaka miwili.
Lakini ni tatizo tu kwa mataifa yanayostawi au wale wanaotoa huduma muhimu za shule.
Hitaji la nafasi nyingi kusoma katika vyuo vikuu pia imekuwa fursa kwa watu kujipatia pesa nyingi sana kwa kutoza ada zisizohitajika.
Kutokana na pesa nyingi zinazohitajika, watu wanalazimika kununua hati bandia za kuonyesha kuwa wamefuzu shahada na tatizo hilo liko nchini Marekani na pia katika mataifa ya kiafrika ikiwemo Kenya.
Shirika la kimataifa la Transparency International linasema kuwa ufisadi umeathiri pakubwa elimu na hata kushusha hadhi ya elimu wanayopokea wanafunzi siku hizi kote duniani.
Hata hivyo kuna habari njema kwenye ripoti hiy: juhudi za kupambana na uifisadi shuleni.
Nchini Chile mafunzo ya kupambana na rushwa yamejumlishwa kwenye mtaala wa shule na nchini Bangladesh walimu hulazimika kuapa kuwa na maadili mema.
Kuwepo kwa simu za mkononi pia kumesaidia watu kuweza kuripoti visa vya ufisadi shuleni.
Pia kuna juhudi za kimataifa kuchunguza matumizi ya pesa za shule.
Lakini ufisadi ungali unaathiri sana bajeti za shule.

Na BBC Swahili

No comments:

Post a Comment