Monday, October 7, 2013

Rais wa Syria Bashar al-Assad amepongezwa na Marekani kwa kutii na kutekeleza azimio la UN na kukubali kuharibi silaha za kemikali zilizotumiwa kuwaua mamia ya watu nchini Syria mwezi Agosti.

Pongezi hizi zimetolewa na waziri wa mambo ya nchi za nje wa Marekani John Kerry.
Kerry alikuwa anazungumza baada ya wakaguzi wa Umoja wa Mataifa nchini humo kusema kuwa silaha hizo tayari zimeanza kuharibiwa.
Juhudi za kuharibu silaha hizo ziliafikiwa katika azimio la UN ambalo lilipitishwa baada ya makubaliano kati ya Urusi na Marekani.
Azimio hilo nalo lilikuja baada ya dunia nzima kulaani matumizi ya silaha za kemikali dhidi ya raia katika kitongoji kimoja karibu na mji wa Damascus.
Marekani hata hivyo ilikuwa imesisitiza kuwa lazima Serikali ya Syria iadhibiwe kijeshi kwa kutumia silaha za kemikali dhidi ya raia wasio na hatia.
Hata hivyo serikali ya Bashar al Assad ilisisitiza kuwa haikutumia silaha hizo na kudai waasi ndio waliozitumia dhidi ya raia.
Madai ambayo yalipingwa vikali na serikali ya Syria na hata kuungwa mkono na Urusi.
Azimio la kuitaka Syria kuharibu silaha hizo liliafikiwa mwezi jana baada ya muda mrefu wa mvutano hulihusu katika Umoja wa Mataifa baadhi ya nchi zikitaka kipengee cha kuadhibu Syria kijeshi ikiwa itakataa kutii matakwa ya UN kuondolewa kwenye azimio hilo.

Taarifa na BBC Swahili

No comments:

Post a Comment