Friday, November 8, 2013

AU yakosoa UN kwa kupuuza Afrika:- Kikao cha Muungano wa Afrika kilichofanyika Addis Ababa mapema mwaka huu Muungano wa Afrika AU umekosoa baraza la Usalama la Umoja wa mataifa

Baadhi ya picha


Kikao cha Muungano wa Afrika kilichofanyika Addis Ababa mapema mwaka huu
Muungano wa Afrika AU umekosoa baraza la Usalama la Umoja wa mataifa kwa kupuuza sauti za Waafrika katika maamuzi yake.
Mkurugenzi wa Baraza la Amani na Usalama la AU El Ghasim Wane anasema wakati mwingi, baraza la usalama hutoa maamuzi bila kuzingatia maoni ya Muungano huo.
Wane ameonya kuwa huenda mapendekezo ya baraza hili yakapuuzwa, iwapo hali itaendelea kama ilivyo.
Wane alikuwa akizungumza kwenye mkutano uliandaliwa kuangazia suala la ufadhili wa mipango ya usalama na amani barani Afrika, lakini suala tata la uhusiano wa AU na baraza la Usalama la umoja wa mataifa, lilijitokeza.
Mkurugenzi wa baraza la amani na usalama la AU El Ghasim Wane, alisema wakati umefika kwa baraza la usalama la umoja wa Mataifa kusikiza kwa makini sauti ya Afrika.
Tetesi hizo zinajiri huku baadhi ya wanachama wa baraza la Usalama la Umoja wa mataifa wakiripotiwa kupuuza ombi la Umoja wa Afrika la kutaka kesi inayomkabili rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, kusimamishwa kwa muda.
Hata hivyo balozi wa Uingereza katika AU Greg Dorey alisema suala muhimu kuhakikisha kuwa uhusiano wa Umoja wa mataifa na AU unaimarishwa.
Huku akitaka muungano huo kuwa katika mstari wa mbele kutatua baadhi ya changamoto zinazokabili bara hili.
Walikuwa wakizungumza katika mkutano wa kujadili jinsi wafadhili wa kimataifa wanavyoweza kuboresha juhudi za AU kukabiliana na changamoto za kiusalama.
Katika mkutano huo, AU ilikiri kuwa inaweza kufanya vyema zaidi katika kukabiliana na vita kama vile nchini Mali na katika Jamhuri ya Afrika ya kati.

Mizengwe' katika uvujaji mafuta Nigeria



Kampuni ya Shell inasema ni wahalifu wanaopaswa kulaumiwa kwa uvujaju wa mafuta Nigeria
Shirika la kimataifa la Amnesty International,limetuhumu makampuni makubwa ya mafuta ikiwemo Shell kwa kuficha ukweli kuhusu kuvuja kwa mafuta nchini Nigeria.
Kwa mujibu wa shirika hilo, makampuni ya mafuta hudai kuwa mafuta huvuja kutokana na njama za watu wala sio wako kukosa uadilifu, ili kukwepa kuwalipa fidia waathiriwa.
Amnesty inasema sababu kuu ya uvujaji, huwa mabomba ovyo au kuu kuu ya makampuni hayo ambayo husababisha tatizo hilo.
Ripoti ya Amnesty inasema kuwa mpango wa kufanya usafi baada ya kuvuja mafuta hayo, huwa ina dosari chungu nzima.
Hata hivyo moja ya makampuni yaliyolaumiwa, Shell, imesema kuwa inakana vikali madai yasiyo na msingi.
Ilielezea tatizo la wizi wa mafuta ghafi, ambayo ilisema ndio moja ya vyanzo vya uchafuzi wa mazingira katika eneo la Niger Delta.
Mwandishi wa BBC mjini Lagos anasema kuwa kiwango kikubwa cha mafuta yanayovuja yamesababisha uchafuzi mkubwa sana wa mazingira katika eneo la Niger Delta na uvujaji unafanyika kwa kiwango kikubwa sana .
Kwa mujibu wa ripoti ya Amnesty, kulitokea visa 474 vya uvujaji wa mafuta mnamo mwaka 2012 katika eneo moja pekee, ambalo linamilikiwa na kampuni ya mafuta ya Nigeria Agip Oil.
Ripoti ya Amnesty imetokana na ushirikiano na mashirika ya kijamii nchini Nigeria kufanya uchunguzi kuhusu visa vya kuvuja mafuta kwa kipindi cha miezi sita.
Ripoti hiyo imesema kuwa hakuna ushahidi wa kutosha kuthibitisha madai ya makampuni hayo kusema kuwa ni wizi na njama za watu ambazo zimesababisha kuvuja kwa mafuta.

Na BBC Swahili

No comments:

Post a Comment