Monday, November 4, 2013

Baadhi ya viti vilivyong'olewa katika ligi kuu wa soka bara kati ya Simba na Kagera Sugar



Baadhi ya viti vilivyong'olewa na mashabiki wakati wa vurugu katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. hali hii inarudisha maendeleo ya soka nchini.

  • Kabla ya kutokea vurugu hizo, mashabiki pia walifanya vurugu Mbeya baada ya kumalizika kwa pambano la Ligi Kuu kati ya Mbeya City na Prisons zote za jijini humo.

Katika pambano la Ligi Kuu ya soka Bara kati ya Simba ya Dar es Salaam na Kagera Sugar ya Bukoba lililofanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam vurugu kubwa zilitokea.
Kabla ya kutokea vurugu hizo, mashabiki pia walifanya vurugu Mbeya baada ya kumalizika kwa pambano la Ligi Kuu kati ya Mbeya City na Prisons zote za jijini humo.
Vurugu za Dar es Salaam zilitokea dakika za mwisho za mchezo uliofanyika Alhamisi iliyopita wakati Kagera Sugar ilipopata penalti dakika za majeruhi za mchezo huo.
Wakati Simba ikiongoza kwa bao 1-0, mwamuzi aliipa Kagera Sugar penalti ambayo iliipatia timu hiyo goli la kusawazisha ambalo liliwafanya mashabiki wa Simba waanze vurugu kwa kuvunja viti na kuvitupa uwanjani.
Bila ya kujali uhalali au uharamu wa penalti hiyo, tunapinga hatua iliyochukuliwa na mashabiki wanaoaminika kuwa ni wa Simba kwani mwamuzi ndiye mwamuzi wa mwisho mchezoni. Uamuzi wa mwamuzi katika mpira wa miguu yanapaswa kukubaliwa na kila aliye uwanjani kwani huo ndiyo utaratibu wa mchezo huo na si vinginevyo.
Ni lazima klabu zitafute njia mwafaka ya kuwasilisha malalamiko iwapo wanahisi kuwa waamuzi kwa njia moja au nyingine hawakuchezesha vizuri na si kujichukulia uamuzi.
Tatizo la waamuzi nchini linapaswa lifuate mkondo mzuri katika kulitafutia ufumbuzi na halitaweza kwisha kwa mashabiki kuchukua hatua mkononi au kufanya vurugu.
Katika vurugu hizo, polisi walifyatua mabomu ya kutoa machozi hali iliyofanya jukwaa lilikuwa na mshabiki waliokuwa wanafanya fujo kuwa mbaya na kwa hiyo kuhatarisha maisha ya watu hasa walemavu ambao hawakuwa na uwezo wa kukimbia.
Hili ni jambo la hatari kubwa kwani yanaweza kutokea maafa kama ilivyowahi kutokea katika nchi zingine duniani zikiwemo za Afrika.
Kila mmoja ni lazima aelewe kwamba Tanzania inaweza kukumbwa na maafa iwapo vurugu za aina hii zitatawala katika viwanja vya soka nchini.
Kuna umuhimu mkubwa kwa viongozi wa klabu kuwaelimisha mashabiki wao kuwa wavumilivu wanapokuwa viwanjani ili kuhakikisha michezo inamalizika kwa usalama.
Inapaswa ieleweke kwamba michezo ni furaha na lengo lake kuu ni kujenga uhusiano nzuri baina ya wanamichezo na si kuleta uhasama.

No comments:

Post a Comment