Monday, November 4, 2013

Serikali yaipongeza timu ya Taifa ya kuogelea Tanzania Swim Squad

  • Tanzania ilitwaa medali 72 kwenye mashindano hayo 22 dhahabu, 25  za fedha, 25 za shaba, huku muogeleaji Hilal
 Serikali imeipongeza timu ya taifa ya kuogelea ‘Tanzania Swim Squad’  kwa kufanikiwa kutwaa medali 72, kwenye mashindano ya Afrika Mashariki yaliyomaliziki hivi karibuni kwenye bwawa la kuogelea la Oshwal  jijini Mombasa, Kenya.
Tanzania ilitwaa medali 72 kwenye mashindano hayo 22 dhahabu, 25  za fedha, 25 za shaba, huku muogeleaji Hilal
Hilal akivunja rekodi kwa kupata medali 15 katika mtindo wa free style mita 50, 100, 200, 400 na 800, butterfly mita 50 na 100, breaststroke mita 50 na 200, backstroke mita 50,100,
Individual Medley mita 100 na 200 na kwenye relay mita 200 freestyle, backstroke na Medley.
Akizungumza katika hafla ya kuipongeza timu hiyo iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, Naibu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo nchini, Juliana Yasoda alisema ushindi huo ni faraja kubwa kwa taifa.
Yasoda alisema  timu hiyo imeonyesha ukakamavu wa hali ya juu kwenye mashindano hayo na kuitaka kuendeleza rekodi hiyo kwenye michezo ya Jumuiya ya Madola ya mwakani na ile ya Cana ya kanda ya nne na ya tano.
“Hatua mliyofika kwenye mashindano ya Afrika Mashariki ni kubwa si tu kwenu nyinyi bali taifa zima la Tanzania, mmetuwakilisha vyema na sisi tunaahidi kuwa bega kwa bega na nyinyi,” alisema Yasoda.
Kwa mujibu wa Katibu msaidizi wa Chama cha Kuogelea Tanzania (TSA), Ramadhan Namkoveka, kikosi cha Tanzania Swim Squad kilikuwa na wachezaji 42 kutoka mikoa ya Mwanza, Arusha na Dar es Salaam.
Namkoveka alisema katika mbizi hizo Tanzania Swim Squad ilitwaa medali katika mitindo ya Backstroke, Breaststroke,  butterfly, Free Style na Individual Medly ambayo ilishindanishwa kwenye mashindano hayo.
“Huo ni mwanzo mzuri kwa timu ya taifa ya kuogelea, hasa baada ya chama kuamua kuweka viwango kwa wachezaji wa timu ya taifa kushiriki kwenye mashindano ya kimataifa na kwa ushirikiano na wazazi tumefanikiwa hivyo mikakati hiyo itaendelezwa kwenye kalenda yetu ya mwakani ambapo tutakuwa na mashindano mbalimbali ya kimataifa,” alisema Namkoveka.

No comments:

Post a Comment